MWALIMU KAZIMBAYA

 



Adeladius Makwega-MWANZA

Mwanakwetu alikaribishwa na mandhari ya mji mdogo wenye nyumba za aina mbili za zamani-kongwe zenye bati zilizoota kutu na nyumba bora za kisasa. Alipozitazama alibaini za zamani zilipigwa bati kitambo hata kuanzia mwishoni mwa mwaka 1969 hadi kuendelea maana alibaini nyumba moja ambayo ilikuwa na jengo kama ya Waajemi ilikuwa na chapa ya mwaka 1971, hii ni nyumba ya zamani, kando yake aliona duka la dawa.

Aliingia dukani hapo nakununua dawa za mafua kwani alipatawa na mafua kutokana na kusafri safari ya vumbi ya saa kadhaa tangu alipopanda basi ndogo pale Hungumalwa.

“Kaka lipa shilingi mia tano tu.”

Dada muuzaji wa duka hili alimwambia mwanakwetu. Hapo dukani alitumia nafasi hiyo kumuuliza mambo kadhaa mhusika huyu ikiwamo ramani ya Mji wa Malya hasa pande zote za dunia Mashariki, Magharibi, Kusini na Kaskazini na maswali mengine lukuki, swali la mwisho lilikuwa pahali lilipo Kanisa Katoliki Malya.Mazungumzo haya na dada wa duka la dawa yalimpa picha kubwa mwanakwetu juu ya eneo hilo kuwa Malya ipo mpakani mwa Wilaya/Mikoa miwili ni Maswa(Simiyu) na Kwimba(Mwanza).

Hilo lilimpa picha pia kuwa mji huo ni wa zamani sana na watu wake wana maandeleo ya muda mrefu hata kabla ya uhuru maana taswira za nyumba bora za bati zilizopata kutu ni za miaka mingi na majengo ya zamani inatoa ushahidi huo huku wakijishungulisha sana na kilimo na ufugaji

Mwanakwetu alitambua kuwa mtu maarufu ambaye ni mzaliwa wa eneo hilo na yupo katika Utumishi wa Umma ni Profesa Eliezer Mbuki Feleshi ambaye aliwahi kuwa Jaji lakini sasa ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Mwanakwetu alitamani kufahamu tabia ya kiongozi huyu kwa nduguze wa Malya-Kwimba na Mwanza.Je anafika kama nduguze wakimtafuta pale wakiwa na shida? “Anapatikana na hata tukiwa na shida tunamueleza na anatusaidia sana.”

Hilo mwanakwetu aliliuza kwa hoja moja kubwa, watu wenye nafasi kubwa wajitahidi kuwa wanafikika kwa urahisi maana wananachi wanaweza wakadhulumiwa haki yao na mtu mwovu, kama yupo mkubwa serikalini wanamjulisha na hilo linaweza kutatulika kwa haraka.

Wananchi wanapoongea na ndugu yao iwe wa kabila moja, imani moja au mahusiano yoyote ya karibu wanaweza kulisema jambo bila woga wala kuhofia chochote. “Ukiwa mkubwa mwanakwetu anakushauri uwe unafikika kwa urahisi na hata wema/ ubaya wa mtu yoyote unaanzia nyumbani kwake.”

Mwanakwetu alikutana na mtu wa pili ambaye alizungumza naye mengi hapa alipata hekima za Wazee wa Kisukuma.

“Mzee wa Kisukuma akishakuwa na ng’ombe katika zizi kubwa na watoto wake wa kike kwa wakiume wakiwa wakubwa zamani walikuwa na desturi ya kukaa yeye na mkewe na kuzungumza,’Mke wangu naona zizi limekuwa kubwa, mimi nakuaga ninaondoka na ng’ombe 200 wewe baki na ng’ombe hizi 300 zako wewe na watoto wako, mimi nakwenda kuazisha mji mwingine.’ Mkewe atamuuliza sasa mimi unaniacha na nani?’Wewe ni mke wangu baki hapa hapa mimi nitakuwa nakuja.’ Huyu baba anaondoka zake na kwenda kuanzisha mji mwingine huko mbali.”

Mwanakwetu akauliza sasa kwanini walikuwa wanafanya hivyo?

“Hekima ya Wazee wa Kisukuma ni kwamba panapokuwepo na mafanikio makubwa shetani huwa anakuwa karibu, unaweza kushangaa mama kampikia mumewe chakula kizuri alafu akamuwekea mumewe kitu cha kufisha akafariki. Hiyo ilikuwa ni busara yao ya kukata zizi.”

Wakiwa katika mazungumzo hayo mara akatokea mama mmoja mtu mzima, mwanakwetu akatambulishwa, mama huyu wa Kisukuma akauliza huyu mgeni ana mke? Ndugu huyu aliyekuwa na mwanakwetu akasema mama muulize mwenyewe. Mama huyu akawa anacheka, tafsri ya kicheko hicho ni kuwa swali limesikika kwa mwanakwetu.

Mwanakwetu kuumaliza mzizi wa fitna akajibu kuwa nina wake wanne. Mama huyu akacheka mno alafu akasema baba hata nafasi hamtuwekei? Mwanakwetu akajibu kuwa katika wake zake wanne atampa talaka mmoja alafu nafasi hiyo atampa yeye. Mama huyu akajibu kuwa hapo haiwezekani, nafasi gani za kutafuta. Mimi nataka kuwa huru ninaona hapo kwako nafasi zilishajaa.

Mwanakwetu aliendelea na shughuli zake hapo Malya akakutana na madaktari wawili falsafa kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, msomi mmojawapo mwanakwetu alimkumbuka kuwa waliwahi kusoma wote, mwanakwetu alipomuona tu alimkumbuka kwa haraka lakini alikaa kimya kuona kama na yeye msomo huyo analikumbuka hilo? Hadi mwanakwetu anatokomea msomi huyo hakukumbuka hilo nadhani ana majukumu mengi ya kusomesha wanafunzi wetu hapo Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, mwanakwetu akasema akikutana naye siku nyengine msomi huyu atamkumbusha.

Uwepo wa mwanakwetu hapo Malya uliendelea sasa alikutana na mwlaimu kijana ambae alitambulishwa ugeni wa Kazimbaya Makwega, Mwalimu huyu alishituka sana, baadaye alimuuliza juu Mwalimu Kazimbaya wa Chilrombora Ulanga Morogoro. Mwanakwetu alijibu kuwa huyu ni baba yake mdogo.

Mwalimu huyu akaomba mkono wa mwanakwetu, mwanakwetu akampa mkono, alafu mwanakwetu akauliza mbona umeomba mkono wangu?

“Yule mzee wakati nikiwa mdogo, baba yangu alistaafu, akatuacha jirani na shule aliyokuwa anafundisha mwalimu Kazimbaya. Baba alituagize tukiishiwa pesa tuwe tunachukua kwa Mwalimu Kaizmbaya, kweli hilo lilifanyika kwa kipindi chote hadi baba akapata pesa zake kustaafu na sisi tukahama hapo, tukio hilo hadi kesho ninalikumbuka, ndiyo maana nimekupa mkono kwa heshimu ya Mwalimu Kazimbaya.”

Mazungumzo ya ndugu huyu yalikuwa ya kidugu mno na baadaye mwanakwetu aliomba nambari ya bodaboda anayemuamini na kweli mwanakwetu alipewa na kijana huyu kufika hapo na kumzungusha eneo hilo la Malya na kubaini kuwa hapo kuna mradi mkubwa wa serikali ulikuwa SGR.Huku Madhari ya ujenzi wa madaraja na tuta la njia za reli na barabara ujenzi ukiendelea.

“Kaka huu mradi umetusaidia mno, hata mzunguko wa pesa sasa ni mkubwa na tunatarajia mradi huu kama ukikamilika maisha ya eneo letu yatakuwa bora zaidi ya sasa.”

Kumbuka msomaji wangu mwanakwetu yupo akizunguka katika eneo hili la Malya, Wilayani Kwimba Mkoani Mwanza.

Je mwanakwetu leo anasema nini?

Kubwa ni umuhimu wa kufanya wema popote ulipo, watu wanaweka kumbukumbu, kumbuka wema wa Profesa Eliezer Mbuki Feleshi kwa ndugu zake. “Anapatikana na hata tukiwa na shida tunamueleza na anatusaidia sana.”. Pia mkumbuke mwalimu wa Chilombora Ulanga Morogoro,“Baba alituagize, tukiishiwa pesa tuwe tunachukua kwa Mwalimu Kazimbaya.”

Mwanakwetu upo?

Kama mema yanawekewa kumbukumbu, kumbuka hata mabaya yanaweza kuwekewa kumbukumbu pia lakini mwanakwetu anasema kumbuka kulipa ubaya kwa wema.

Nakutakia siku Njema.

makwadeladius@gmail.com

0717649257

0/Post a Comment/Comments