ASKOFU ALIYEMUANDIKIA MWANAKWETU BARUA

 


 



Adeladius Makwega-LUSHOTO

Siku ya Aprili 29, 2022 Mwanakwetu alikuwa katika Mji wa Lushoto, mkoani Tanga. Mandhari ya mji huu ilikuwa ya baridi kali, manyunyu na mvua kubwa. Kwa kuwa alifika katika ofisi mojawapo iliyokuwa katika majengo ya Halmashauri hii ambayo sasa imepangishwa ili wajiongezee kipato. Wakati narudi kutoka huko alipita kandokando ya Kanisa Katoliki la Ekaristi Takatifu Lushoto Mjini Jimbo Katoliki la Tanga, kwa pembeni kuna nyumba ya makazi ya mapadri alishuhudia vibanda kadhaa vizuri kuzunguka nyumba hii.

Vibanda hivyo vilimvutia mno kwani vimebadilisha mandhari ya eneo hilo kutoka kichaka na kuupamba vizuri mji huu mkongwe ambao una Ikulu ya kwanza iliyojengwa na Mjerumani.

Alipokuwa anatazama vibanda ambavyo ujenzi wake ulipitia hatua kadhaa za changamoto mara bomoa mara wekwa alama X lakini sasa vimekamilika kwa ushirikiano wa waamini wa kanisa hilo na viongozi wao.

 

Mwanakwetu akiyaona manufaa mengi ya vibanda hivyo,

 

“Vinameondoa kichaka cha wigo mjini na kuwa urembo unaopendezesha sehemu ya mji huu. pia kuliongezea kipato kanisa hilo na tatu, kuongeza idadi wa wafanyabishara katika mji huu. Nne, hata kuongeza bidhaa zinazouzwa Mjini Lushoto. Tano kusogeza huduma jirani na jamii na kupunguza safari za wateja kwenda mbali kufuata bidhaa hizo na Sita kuongeza mzunguko wa pesa katika eneo hilo.”

 

Mandhari ya vibanda hivyo ilimkumbusha Mwanakwetu namna Kanisa Katoliki Jimbo la Tanga linavofanya miradi kadhaa ya maendeleo ikiwamo ya elimu, afya, ufugaji na kilimo inayosimamiwa na mapadri na watawa kwa miaka mingi katika eneo hili lililopo Kaskazini Mashariki mwa Tanzania.

Mwanakwetu akiwa anazunguka mji huo huu aliikumbuka barua moja ambayo aliwai kuandikiwa na Baba Askofu Antony Banzi wakati wa uhai wake mwaka 2017/2018 ambayo ni yake ya kwanza kuandikiwa na Baba Askofu katika maisha yangu.

 

“Mtu mdogo kama mimi kiimani na kwa kila kitu inawezaji kupokea barua kama hii yenye tafakari nzito kutoka kwa Baba Askofu Banzi na kusainiwa na yeye mwenyewe?”

 

Barua hiyo haikuwa na maelekezo ya kiroho wala barua ya maombi ya kitu chochote kwa Mwanakwetu bali kwa nafasi yake ilikuwa barua ya tafakari kutoka kwa Baba Askofu kwenda kwa mtu mdogo sana Mwanakwetu.

 

“INAWEZEKANA,TIMIZA WAJIBU.”

Hayo yalikuwa maneno yaliyonukuliwa na Askofu Banzi si kutoka kwa kauli mbiu ya TANU ya Julius Nyerere na Oscar Kambona la hasha bali alibainisha kuwa amekuwa akifuatilia kauli mbiu hii ambayo imekuwa ikibaki katika kila Kitabu cha Wageni kinachosaini iwe mjini au kijijini na Mwanakwetu.

 

“Katika maisha ya binadamu na hasa kwa kijana, jukumu lako ni kufanya kazi kwa bidii sana na usikatishwe tamaa na mtu yoyote yule kwa kuwa inawezekana kukamilika kwa kutimiza wajibu tu kama kauli yako mbiu.”

 

Alisema Baba Askofu Banzi katika barua hiyo yenye kurasa mbili za maandsihi.

Baba Askofu Antony Banzi ambaye alikuwa Askofu wa Jimbo Katoliki la Tanga kwa miaka 26 tangu alipoteuliwa Juni 24, 1994 na kutawazwa rasmi septemba 15, 1994 aliufanya utume huo hadi alipofariki dunia Disemba 20, 2020.

 

“Mwanakwetu alitafakari mno barua hiyo lakini akibaki na maswali mengi juu ya Askofu Banzi. Je aliwezaje kuyaona maandishi yangu kadhaa ya vitabu vya wageni vilivyokuwa vinaandikwa kauli hii ya TANU na kusaini saini ya Mwanakwetu katika maeneo mbalimbali ya ofisi za vijijini, mitaa na kata alizozitembelea kati ya mwaka 2016-2018 katika Halmashauri ya Lushoto?”

 

Swali hilo Mwanakwetu anatambua fika haliwezi kujibiwa na Askofu Banzi ambaye sasa amelala usingizi mzito kaburini.

 

“Mwanakwetu akiwa njiani kueleka alipofikia alibaini kuwa kanisa si majengo yanayoonekana kwa ajili ya kusali tu kanisa ni jamii husika ambayo inakaa pamoja ikifanya kazi mbalimbali za maendeleo ili kuistawisha jamii hiyo.”

 

Mnapofanya kazi hizo za ustawi wa jamii mnakutana na mnafahamiana vizuri, siyo lazima ukutane na Baba Askofu bali unaweza kukutana na mwingine ambaye mtafahamiana huyo akakuelezea kwa mwingine namna ulivyo iwe kwa mema au kwa mabaya.


Japokuwa Baba Askofu Antony Banzi amelala kaburini, leo hii Mwanakwetu ameamua nimeamua ahuishe nafsi yake katika ulimwengu wa fikra kwa yule anayejaliwa kuisoma matini hii na kuzitazama kwa ndimi zake baadhi ya kazi alizozifanya akiwa hai katika Jimboni Katoliki la Tanga katika ustawi wa binadamu. Mwanakwetu anakumbuka kauli mbinu yake iliyobebwa na maneno matatu HEKIMA, UMOJA na AMANI na ana hakika vitatamalaki katika kila eneo lenye mapenzi mema kuanzia Jimbo Katoliki la Tanga, Tanzania na kwingineko ulimwenguni ambapo kwa miaka yote 26 ya Uaskofu wake mbegu hii imepandwa.

 

“Raha ya milele uumpe ee Bwana na mwanga wa milele umuangazie, apumzike kwa amani, amina.”

 

Mwanakwetu anatambua fika kuwa kwa sasa bado JImbo Katoliki la  Tanga ahalipata aAskofu wake , kitendo cha kuyakumbuka meme ya kiongozi huyu wa kiroho Mwanakwetu  anaendelea kusali sala zake ili jimbo Katoliki la Tanga kupta  Askofu wake , huku akimwomba balozi wa baba Mtakatifu nchini  kumkumbusha hilo, hili Baba Mtakatifu Fransisko amchague Askofo wa Jimbo hilo.

 

makwadeladius@gmail.com

0717649257





0/Post a Comment/Comments