SAMEHE HARAKA WALA USICHELEWE

 


Adeladius Makwega-MWANZA

Aprili 29, 2023 Mwanakwetu alikwenda kusali jumuiya, alipotoka huko alirudi nyumbani kwake, akiwa hapo alifanya usafi kidogo wa nguo zake na alipomaliza, akaichukua simu yake iliyokuwa katika chaji, alipoifungua simu hiyo alikutana na ujumbe na picha mbalimbali katika makundi kadhaa yaliyomo katika simu hiyo.

Picha mojawapo aliyoiona iiimuonesha mwanahabari Yotham Ndembeka, rafiki wa Mwanakwetu, Kada wa CCM wa miaka mingi wakiwa na tabasamu moja zuri na mzee wetu Bernad Membe.

Mwanakwetu aliitazama picha hiyo kwa umakini mkubwa, alitafakari na aliliona wazi wazi tabasamu la mzee Membe (Mzee wa Londo-Mzee wa nimtoe nisimtoe?) Mwanakwetu huku akiikodolea picha hiyo aliyakumbuka mambo makubwa mawili: kwanza ni simulizi ya mtumishi wa benki huko mikoa ya kusini mwa Tanzania na simulizi ya pili ni ya mafundisho yake ya Komuniyo ya Kwanza mwka 1988.

Kwa kuanza msomaji wake anaomba asiwe mchoyo aanze na simulizi ya mtumishi wa benki huko mikoa ya kusini mwa Tanzania,

“KIjana mmoja Mkwere alikuwa akifanya kazi mikoa ya kusini mwa Tanzania, nyumbani kwa mheshimiwa Bernad Membe. Kijana huyu alifuata na mtu aliyekuwa na shida ya kuuza eneo lake, kijana wa benki hakuwa na fedha, hivyo aliiomba benki yake anapofanya kazi mkopo na kuchukua fedhai hizo na kulinunua eneo hilo. Kijana huyu alikuwa bado kijana sana, hakuwa na majukumu ya mke na watoto. Hivyo alipata eneo hilo zuri sana ambalo lilikuwa kando na Bahari ya Hindi. Eneo hilo kijana huyu alinunua kwa ngekewa tu maana muuzaji alikuwa na shida hivyo mtumshi wa benki alibahatisha kulipata eneo hilo na kulipa pesa zote taslimu. Kutokana naeneo hilo kuwa nzuri mheshimiwa Bernad Membe alivutiwa na eneo hilo, hivyo mheshimwa wetu alimtuma mtu wake wa karibu kuulizia eneo hilo ni la nani? Majibu yalipatikana kuwa ni la kijana anayefanya kazi benki ndiye mmmiliki halali wa eneo hili makini. Mheshimiwa Bernad Membe alimtuma mtu wake wa karibu kumfuata kijana huyu kuwa Mzee Londo amelihusudu eneo hilo hivyo anataka kulinunua kwa bei atakayotaja kijana huyo wa Benki. Kijana wa Benki alipofuatwa alimpokea mjumbe akamsikiliza akamjibu mjumbe kuwa yeye hauzi eneo hilo. Mheshimwa Membe alijaribu kumbembeleza kijana huyo lakini kijana huyu alikata kuliuza. Alifuatwa mtu mwingine kumshawishi kijana huyo lakini, mheshimiwa wetu aligonga mwamba kulinunua eneo hilo hadi kesho na yule kijana wa benki hadi hii eneo lake na amejenga makazi yake ambayo amepangisha .”

Mwanakwetu alipouliza je mheshimiwa Membe hakutumia uaskari kanzu wake na Uwaziri wake kukutisha ? Kijana alijibu kuwa hakufanya hivyo, japokuwa kijana wa benki uwoga ulimuingia lakini mheshimwa Bernad Membe hakufisidi.



Mwanakwetu akamuuliza kama angefanya hivyo ungefanyaje?

“Nilipanga kumfuata mheshimiwa Jakaya Kikwete nyumbani kwake, kama wangenisumbua.”

Mwanakwetu alipoitazama picha hiyo pia aliyakumbuka mafundisho ya Komuniyo ya Kwanza akiwa kijana mdogo akifundishwa na Watawa wa Shirika la Dada Wadogo Kanisa la Mtakatifu Antony wa Padua, Parokia Mbagala Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam enzi hizo .Mtawa aliyefundisha mafundisho hayo aliitwa Sista Getruda aliwambiwa maafunzo haya.

“Ni jambo la kawaida mno pale mtu anapoumizwa au kukerwa na mtu mwingine kukasirika, maana hasira inakuja kutoka ndani yako, na hasira hizo zinaweza kuibua mambo mengine ikiwamo kutaka kulipiza kisasi. Wakati hasira hiyo inazidi inaweza kuwahusisha na watu wengine ambao hawakuwapo katika shida hiyo. Hiyo ni hatari na ndiyo maana Biblia inaitaja hasira ni sumu.”

Haya yanaelezwa bayana katika kitabu cha Waebrania 12: 15 ,

“Angalieni sana mtu ye yote asishindwe kupata neema ya Mungu, na muwe waangalifu pasizuke chuki ambayo, kama mmea wenye sumu, inaweza kukua ikaleta matatizo na kuwachafua wengi.”

Msomaji wangu kuwa makini, je unapenda sumu hiyo ikuumize wewe na wale walio jirani na wewe? Mwanakwetu alilkumbuka kuwa Biblia inakwenda mbali zaidi katika Waefeso 4.31,

“Ondoeni kabisa chuki yote, ghadhabu, hasira, ugomvi na matusi, pamoja na kila aina ya uovu. Muwe wema na wenye mioyo ya upendo kati yenu, na kusameheana kama Mungu alivyowasamehe kwa ajili ya Kristo, Watoto wa Nuru.”

Msomaji wangu Mwanakwetu aliendelea kuyakumbuka haya, je unawezaje kumsamehe huyo aliyekukosea? Mafundisho ya Mwanakwetu Komuniyo ya Kwanza anakumbuka kuwa watawa hao walisema kuwa , KIla mmoja atambue umuhimu wa msamaha ambopo Yesu aliutilia maanani mno wakati anawafundisha wanafunzi wake namna ya kuongea na Mungu (kusali) rejea Matayo 6,12.

“Na utusamehe makossa yetu kama na sisi tulivyokwisha kuwasamehe waliotukosea.”

Mafundisho ya Ukristo yanaelekeza kuwa ni lazima kila Mkirsito amkatae shetani, rejea Waefeso 4, 26-27

“Kama mkikasirika, msikubali hasira yenu iwafanye mtende dhambi, na wala msikae na hasira kutwa nzima. Msimpe ibilisi nafasi.”

Mwanakwetu alikumbuka kuwa Ukristo unakwenda mbali zaidi, rejea Wakosai 3.13.

“Mkichukuliana, na kusameheana, mtu akiwa na sababu ya kumlaumu mwenzake: Kama bwana alivyowasamehe ninyi, vivyo na ninyi.”

Mwanakwetu akachukua simu yake na kuiweka katika begi lake huku akitabasamu kama tabasamu la mzee Membe akafunga mlango na kuondoka zake.



Je siku ya leo Mwanakwetu anasema nini?

Kama kilivyosimuliwa na kisa cha yule wa kijana wa Kikwere wa benki juu ya Mheshimiwa Membe hakutumia cheo chake na wala uaskari kanzu kumtisha yule kijana ambaye alikuwa hauzi eneo lake. Katika ulimwnegu wa sasa wapo watu wanaotumia uaskari kanzu wetu na vyeo vyetu kuwatisha wengine hilo halikubaliki. Bernad Membe ni mtu mzuri sana alikuwa anatambua kuwa Uaskari kanzu na Uwaziri wake ni dhamana tu hiyo  ni mali ya Watanzania, hilo ni jambo zuri linapaswa kuigwa na kila mmoja wetu ambaye atajaliwa kuisoma matini haya.

Katika kisa cha Mafundisho ya Komuniyo ya Kwanza ni kukumbushana kumsamhe mwenzako aliyekukosea maana huo ndiyo Ukristo. Ndugu yangu tambua msamaha wa Mungu kwako? Je unatambua na kuiheshimu sadaka aliyoitoa Bwana wetu Yesu Kristo Msalabani? Yesu alifanya hivyo ili mimi na wewe tusamehewe dhambi zetu. Je unaiheshimu sadaka hiyo ? Msomaji wangu usisite, samehe haraka na wala usichelewe.

Mwanakwetu kwa heshima zote anawashukuru mno na kwa pamoja Yotham Ndembeka na mheshimiwa Bernad Membe kwa picha hiyo nzuri iliyosaidia kujenga tafakari hii.

makwadeldaius@gmail.com

0717649257



 

0/Post a Comment/Comments