MSISITE KUIKAGUA MIRADI SERIKALI KUU.


Adeladius Makwega MWANZA

Serikali imesema kuwa Chama cha Mapinduzi (CCM) ndicho chenye miradi yote ya Serikali Kuu na Serikali za Mitaa hivyo kisisite na kinapaswa kushirikishwa katika hatua zote ili kiwezo kutoa maoni na ushauri wake wakati wa utekelezaji.



Hayo yamesemwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza ndugu Balandya Elikana akiwa Malya Wilayani Kwimba wakati akitembelea miradi kadhaa ya maendeleo katika mkoa huo ambayo inatekelezwa kwa nguvu za wananchi, Serikali za Mitaa na Serikali Kuu, Juni 30, 2023.

“Diwani wa CCM upo? Unaufahamu huu mradi? Je unafuatilia utekelezaji wake? Unautambua kuwa huu ni mradi wako? Pale pesa zinapochelewa usisitwe kufika katika ofisi yangu ili tuweze kutambua shida ni nini? Na nani anakwamisha hilo. Jambo hili ninalisema si Malya tu bali mkoa mzima wa Mwanza katika miradi yote, iwe ya Serikali Kuu au Serikali za Mitaa.”

Katibu Tawala Elikana alionekana akiambatana na viongozi kadhaa wa mkoa huo kutoka kamati mbali ikiwamo Kamati ya ulinzi na Usalama waliovalia sare za majeshi yetu mbalimbali ; JWTZ, Jeshi la Polisi, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji , Jeshi la Magereza na Askari Kanzu kadhaa.

Msafara huu uliombatana na kiongozi huyo ulionekana wakikagua miradi kadhaa katika Wilaya ya Kwimba ambapo walipofika Chuo cha Maendeleo ya Michezo Malya walikagua Jengo la Hosteli la wanachuo ambao ni mradi wa bilioni kadhaa unaogharamiwa na Serikali Kuu ambapo kwa sasa jengo hilo lipo katika hatua nzuri.



Akizungunza katika lugha ya kushauri, wakatii mwingine akitoa maagizo ya serikali kwa kutumia lugha ya staha na heshima mara kadhaa kiongozi huyo Mkoa wa Mwanza alionekana kushirikiana kwa karibu na aliongozana nao.

“Hapo mmeona pana marekebisho, itabidi mfanye marekebisho hayo mapema eeeh…! Tunaziomba hizo taarifa mapema, mna imani kuwa huu mradi utakamilika mwaka wa fedha wa 2023/ 2024?. Natambua hapa sisi serikali tumeweka pesa nyingi.”

Katika ziara hiyo, wakiwa katika mradi wa Hosteli ya Chuo cha Maendeleo ya Michezo Malya walitumia zaidi dakika 79 huku Mkuu wa Chuo cha Maendeleo ya Michezo Malya Richard Mganga akijibu maswali kadhaa na ufasaha mkubwa pia akipokea maelekezo kadhaa ya serikali yaliyotolewa ziarani hapo.

Mara baada ya dakika 80 kutimu, ugeni huo uliingia katika motokali zao zilizoongozwa na vIjana wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza,walionekana wakipanda Toyota Land Cruizer-I hz kwa ukakamavu mkubwa na kuongoza msafara huo.



Mwandishi wa taarifa hii akiwa kandoni ya ugeni huo alitumia fursa hii na alizungumza na viongozi kadhaa wa CCM kutoka Kata ya Malya waliovalia sare za CCM akiwamo Bi Hawa Salehe ambaye alijitambulisha kama Katibu Kata CCM Malya huku akisema,

“Nashukuru kwa maelezo hayo ya Serikali na namshukuru mno Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza kwa kututambua , kwa kufika Malya na maaagizi yake yote, kata ya Malya itatekeleza kama yalivyoelekezwa. Tutajipanga na Diwani wetu kuhakikisha tunapokagua miradi ya Kata yetu na miradi yote ya Serikali Kuu katani itaingizwa katika orodha na kukaguliwa ipasavyo.”

Mwandishi wa ripoti hii pia alibaini kuwa Bi Hawa Binti Salehe aliambatana na Diwani wa Malya mhe. Atanas Niga, Katibu Mwenezi wa Kata ndugu Mohamed Mangwela na Mwenyekiti wa Vijana Kata ndugu Manyunga Kidoyayi.



0/Post a Comment/Comments