Hodari Kuchanja Mbuga za Maendeleo Tangamano


MASHAKA MHANDO-TANGA &Adeladius Makwega-MWANZA

“Husna hana shida, kwa hakika ameayagusa mno maisha yangu na bila ya yeye hata hii biashara ninayoifanya hii nisengekuwapo hapa, sasa hibi nimeacha kufanya vibarua bali nina biasahra yangu mwenyewe, maana amenishika mkono na siyo mimi peke yangu bali ni wengi.”

Hayo ni maelezo ya Jamila Ngogo mkazi wa Vuri Lushoto,Mkoani Tanga akizungumza wakatia makala haya yakitayarishwa.



Maelezo ya Bi Jamila yananukuliwa mwanzoni kwa sababu nyingi maana hivi karibuni mbunge huyu wa viti maalumu mkoani Tanga, ametembelea vikundi vya akina mama vilivyokopeshwa fedha kupitia asilimia 10 ya mapato ya ndani ya Halmashauri ya Jiji la Tanga. Mbunge huyo amekuwa karibu na Wanawake wengi mkoa wa Tanga kutokana na kufanya kazi kwa pamoja na kidugu, alitembelea vikundi vya ufugaji kuku, usagaji nafaka pamoja na uuzaji wa unga wa chakula , hiyo ikiwa ratiba yake kila akitoka Bungeni.

Akizungumza na akina mama hao katika kikao kilichofanyika Kata ya Mnyanjani na kisha mkutano kule Mabokweni ambako alizungumza na wananchi wa Kata za Nguvumali na Chumbageni alisema,

”Mikopo waliyopewa vikundi hivyo vya ujasirimali watumie pesa hizo kujenga uchumi wao na kupiga hatua kimaisha.”

Aliongeza kuwa fedha walizopewa zinatakiwa zirejeshwe ili ziweze kukopesha wajasirimali wengine kwa kuwa dhamira ya serikali ni kuwasaidia ili waweze kuinuka kiuchumi. Hata hivyo, alisema mikopo hiyo inayotolewa na serikali asilimia nne vijana na wanawake na asilimia mbili makundi ya watu Wenye ulemavu, kwasasa imesitishwa ili kuboresha kwa makundi hayo tofauti na awali. Mbunge huyo aliipongeza Halmashauri ya Jiji la Tanga kwa kuweza kutoa fedha nyingi za mikopo tofauti na maeneo mengine aliyopita baada ya kukuta kikundi kimoja kimepewa mkopo wa zaidi ya shilingi milioni 40.

"Kiukweli nimetembea wilaya nyingine na hata kule kwetu Lushoto hakuna mjasiriliamali ambaye Halmashauri imeweza kumkopesha fedha kama hizi sana sana huko wanawakopeshwa shilingi milioni mbili au tatu,"

Kinagaubaga aliwaambia akina mama hao kuwa fedha hizo wasione zinatolewa tu kwa bahati mbaya bali ni usimamizi mzuri wa mbunge wa jimbo la Tanga Ummy Mwalimu ambaye pia ni Waziri wa Afya.

"Muungeni mkono mbunge wenu (Ummy) ni kiongozi makini na ndiyo maana ameaminiwa na kupewa uongozi, mnaweza msione umuhimu wake lakini nawaambia mshikeni sana mbunge wenu."

Mhe Husna katika ziara yake katika jimbo la Tanga shabaha yake ilikuwa ni kukutana na wananchi na kujua changamoto zao lakini pia kuwaomba wananchi wamuunge mkono Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kutokana na kazi nzuri anayoifanya nchini ikiwemo mkoa wa Tanga. Kwani kina mama wanao wajibu mkubwa wa kumuunga mkono Rais licha ya kuwa mwanamke mwenzao lakini ametekeleza miradi mingi ya maendeleo nchini katika sekta za afya, elimu, maji na miundo mbinu.



Wakizungumza kwa nyakati tafauti akinanana kadhaa wa mkoa wa Tanga ambayo mawazo yao yanafanana na ya Jamila Ngogo wa Lushoto ambayo yanaonekana mwanzoni mwa makala haya wanasema,

“Dada Husna anachapa kazi sana, ameendelea kutuunganisha wanawake wote wa mkoa wa Tanga na kila mara tunapomuhitaji afike katika kufungua vikoba vyetu na hata katika magawiwo ya fedha za vikundi vyetu amekuwa hodari sana wa kufika na kutuongezea nguvu na kutushika mkono.”

Hayo ni ya Bi Aisha Mlelwa wa Mkinga.

“Tulikuwa hatuna kikundi, mh Husna alifika hapa, akatuhamasisha vizuri na kuweza kuanzisha kikundi chetu, mwongozo wake umetujenga vizuri, sasa tunasifa zote, tumeambiwa na Halmashauri yetu ya Korogwe Mji chini ya mkurugenzi wake Tito Mganwa kuwa tutapata fedha katika mgao wa robo ya pili ya mwaka wa fedha 2023/ 2024, hakika.Mhe .Husna Sekiboko ni hodari na kuchanja mbuga za Maendeleo ya Tangamano.”

Alisema Rehema Madenge mkazi wa Mji wa Korogwe.

Mhe. Sekiboko aliingia Bungeni kwa mara ya kwanza mwaka 2020, kitaaluma ni mwalimu mwenye Shahada ya Kwanza ya Elimu ya Sayansi ya Siasa na Historia kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, mzaliwa wa Lukozi Lushoto mkoani Tanga. Kabla ya kuwa mbunge aliwahi kufanya kazi kadhaa ikiwamo Ualimu katika shule za kutwa mbili za Masasi na Shekilango na baadaye akateuliwa kuwa Katibu Tawala wilaya mojawapo ya mkoa wa Lindi.




 

0/Post a Comment/Comments