SHEMASI MAGIRINI




Adeladius Makwega-MWANZA

Mwanakwetu alikuwapo nyumbani kwake, hiyo ikiwa jioni ya Agosti 18, 2023, hapo katulia tuli keshamaliza kuusoma waraka wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania, wakati akisoma waraka huo wenye kurasa 8 mwanzoni moyoni alijiuliza kwanini waraka huu umetolewa kwa kuchelewa ?

Baadaye swali hilo lilijibiwa na maelezo ya kina ya waraka huo ambapo ulionesha kulikuwa na majadiliano baina ya TEC na upande uliombwa kufanya maamuzi.

Huku Mwanakwetu akisema moyoni,

“Waraka huu unapousoma unaweza kujiuliza maswali na kujijibu wewe mwenyewe kadili unavyousoma, maana unajieleza wazi wazi.”

Mwanakwetu wakati anausoma alikumbuka aina nne za usomaji,

“Skimming, Scanning, Extensive na Intensive Reading.”

Kumbuka msomaji wangu Mwanakwetu yu nyumbani kwake na alipousoma waraka huo alitumia Intensive Reading, akawa anautafakari moyoni.

Mara akaingia katika kundi mojawapo la mitando ya kijamii na kukutana na mijadala juu ya waraka huo kutoka kwa wadau mbalimbali wakitoa maoni yao, Mwanakwetu akayasoma vizuri wengine wakimshambulia Padri Kitima, Mwanakwetu akasema hayo siyo mawazo binafsi wa Padri Kitima bali ni msimamo wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzamia na ukurasa wa saba na wanane unajibu hilo kwa orodha ndefu wa MABABA WALIOKETI katika jambo hilo kutoka 1-37-Kutoka Askofu Mkuu Gervas Nyaisonga hadi Askofu Mteule Thomas Kiangio.



Pia Katika kundi hilo Mwanakwetu akakutana na maneno haya,

 “Shemasi hata upadri hajakaribia !”

Wadau wa kundi hilo wakawa wanatiririka kwa sentensi tele, mwingine akasema,

“Basi wamfukuze.”

Mwanakwetu anaendelea kusoma ujumbe unaofuata ambapo mdau mwingine akasema,

“Ni daraja dogo sana, unajiondoa mwenyewe tu, haufukuzwi.”

Maoni yanaendelea kuporomoshwa na huku mdau mmojawapo miongoni wa mwenye maoni hayo juu akaugeuza usikani gafla , akasema maneno haya ,

“Ana haki ya kutoa maoni yake, pia he is a free man, hafungwi na Kanisa.”

Msomaji wangu Mwanakwetu anaendelea kusoma kila ujumbe unaofuata, sasa akaibuka mdau mwingine,

“Shemasi vs Maaskofu? Hamna shemasi humo.”

Msomaji wangu Mwanakwetu anaendelea kusoma ujumbe huo huku akicheka kwa sauti maana awali alikuwa anachekea moyoni na sasa akaibuka mkubwa mwingine akaja na hili,

“Hakuna shemasi humo, hapa Shemasi magirini, from the factory.”

Msomaji wangu kicheko cha Mwanakwetu kikaongezeka, kumbuka wadau wa kundi hilo ambalo ni la wasomi wenye shahada za elimu mbalimbali wanafunguka, wengine wanatuma michoro na picha za ishara ya kucheka na kukubaliana na hoja zinazotolewa kwa wajumbe wote wanaotoa mawazo yao.



Hiyo sasa ni saa mbili usiku, mara Mwanakwetu akabanwa na njaa na kiu ya maji, kwa bahati mbaya na nyumbani kwake hakukuwa na kitu, alitoka nyumbani kwake na kwenda kununua chakula na maji ya kunywa.

Msomaji wangu hapo pahala anapoishi muungwana Mwanakwetu kila akielekea dukani na mikahawani lazima apite Kanisa Katoliliki jirani ambalo lina ukumbi mkubwa unakodishwa kwa watu wenye harusi na sherehe mbalimbali.

Akiwa anapita kando na Kanisa hilo akausikia wimbo huu ukumbini,

“Ingekuwa hivyo wezi wangeenda,

Ingekuwa hivyo wachawi wangeenda,

Ingekuwa hivyo waongo wangeenda,

Bwana…

Bwana wa Bwana hapokei rushwa,

Bwana wa Bwana hapokei rushwa…”

Wimbo huo unaimbwa ukumbini naye Mwanakwetu akawa anapita njiani kuelekea mkahawani mkononi akiwa na tochi nyeusi huku sasa na yeye akivutiwa kuimba kiitikio cha wimbo huo,

“Bwana wa Bwana hapokei rushwa.”

Mwanakwetu akiimba kiitikio hicho huku boda boda na baiskeli zikimpita kwa kasi mawazo yake ni kuwahi kula mkahawani.

Mwanakwetu upo?

Mwanakwetu alifika mkahawani kula na baadaye dukani na kuyanunua maji kisha kuianza safari ya kurudi nyumbani kwake, huku akilini mwake akiukumbuka mno ule mjadala wa shemasi yule aliyepachika jina la Shemasi Magirini.

Nakutakia siku njema.

makwadeladius@gmail.com

0717649257

















0/Post a Comment/Comments