TEMBELEENI WAHITAJI-MIZENGO PINDA

 



Adeladius Makwega-Pugu&Malya.

Waziri Mkuu Mstaafu wa awamu ya nne wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mhe. Mizengo Pinda amesema kuwa zamani kwake ilikuwa ngumu kukumbuka kuwa imefika siku yake ya kuzaliwa lakini muda ulivyokuwa unasonga akawa anapata ujumbe kuwa leo ni siku yako ya kuzaliwa kutoka kwa watu mbalimbali, jambo hilo linampa faraja sana.

Hayo yamesemwa na mhe Pinda Agosti 27, 2023 nyumbani Kwake Pugu Jijini Dar es Salaam alipotembelewa na kundi na vijana kadhaa waliowahi kuguswa kwa namna mbalimbali katika maisha yao na kiongozi huyu mstaafu.

“Ninawashukuru mno kwa niaba yangu na mama Tunu kwa kufika hapa kwangu na kutukumbuka,, kwa mawazo nilitamani tukutane hapa, ni jambo zuri, kwani Mungu ametujalia uhai, najua mpo katika shughuli mbalimbali za kutafuta riziki, siku ya kuzaliwa siyo lazima ifanyike siku ile ile, kuisogeza mbele siyo shida , nawashukuru kwa zawadi zenu mlizonipatia. Natambua na kuheshimu sana zawadi hizi, Unapopewa zawadi usiitazame tu ile zawadi, bali natazama ule upendo wenu kwangu na kwa mama Tunu, kwa kutukumbuka, mkaanza kuhangaika na kuzitafuta hizi zawadi, Mungu awabariki sana.”

Akiendelea kuzungumza mbele ya wawakilishi wa kundi la vijana hao karibu 200 Mhe Pinda ambaye alitimiza miaka 75 Agosti 12, 2023.aliongeza kuwa,

“Moyo wenu huu napenda uwasaidie wengine ,msaada kwa mwingine si utajiri, ni ile hali ya kujipima wewe na yule unayemsaidia, hicho ni kitu kikubwa sana, unaweza kuwa na mashati 18 mengine umeyaacha tu wala hayavaliwi, lakini yupo mtu anahitaji shati moja tu. Jamani yakusanyeni yapelekeni kwa wazee hao, yapelekeni kwa wahitaji. Huo ni moyo wa upendo hiyo ni karama, Mungu kakupa unatakiwa uitumie kusaidia wenzako. Fanyeni hivyo hata katika mazingira mnayoishi, kuna bibi na babu wengi wanaishi katika mazingira magumu. Usingoje bibi/ babu huyo aseme anaomba hiki na kile, kusanya shati na doti ya khanga mpeleleke mara moja na atakushukuru kweli kweli.

Akizugumza kwa unyenyekuvu mkubwa kama mtu ambaye hakuwa na mamlaka yoyote, akitamka neno kwa neno mbele ya vijana hao mhe Pinda alisisitiza kuwa,

“Ninawaombeni sana kila mmoja, kwa nafasi yake, kila wakati na kila mwaka muwawatembelee na kuwasaidia wahitaji sambamba na siku yangu ya kuzaliwa.”



Mara baada ya mhe Pinda kusema hayo Mwenyekiti wa vijana hao ndugu Edward Clement Kyungu alisimama na kusema haya,

 “Tunakushukuru sana kwa kutupokea, tunakushukuru sana kwa kutukumbuka, tunakutakia maisha mema, tumeyapokea yote uliyoyasema na tutayatekeleza kwa vitendo na uhodari mkubwa, Mungu akubariki kwa kutimiza miaka 75 ya kuzaliwa.”

Vijana hao kwa pamoja waliimba wimbo wa kuzaliwa, wakakata keki na kupiga picha ya pamoja.

(Mwenyekiti Kyungu)


Mwenyekiti Kyungu aliambatana na viongozi wenzake akiwamo Make Apolinari Nyema (Mhazini), Vivian Nyanjala Mtebe (Katibu) na Lilian Phidelis Mwidunda( Makamu Mwenyekiti) .

Mwadishi wa ripoti hii alivutiwa sana na sebule ya kijamaa ya mhe Pinda huku ikipambwa na picha moja kubwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi mhe.Samia Suluhu Hassan iliyoonekana amevalia mavazi yake rasmi ya CCM.


(Makamu Mwenyekiti Liilian Mwidunda)

(Picha ya ilivyomvutia mwandishi)

0/Post a Comment/Comments