HODARI WA KUKAA NA NYATI

 




Adeladius Makwega-MWANZA

Mwaka 1972 ndugu S Kazi ambaye anajitambulisha kama alikuwa mwalimu na mzaliwa wa Usukumani alizunguka maeneo kadhaa ya Usukumani kama vile Maswa, Shinyanga na Mwanza kufanya tafiti nying juu ya kabila lake hilo.

Ndugu S Kazi anaeleza wazi wazi kuwa katika safari hizo hali ya usafiri ilikuwa ngumu sana ambapo maeneo mengi alisafiri kwa kutumia punda, baiskeli na mara chache kupanda malori na mabasi kutoka eneo moja kwenda lingine.

Msomaji wa Mwanakwetu nakuomba utambue kuwa ndugu Kazi amefanya tafiti nzuri zenye simulizi nyingi za Wasukuma ambazo mara nyingi ndugu yetu Mwanakwetu anazinukuu kama zilivyo.

Ndugu Kazi katika ukurasa wake 187 katika kitabu kimoja kikubwa kilichokusanya tafti kadhaa za makabila ya Tanzania kikiwa na jina Utani Relationships in Tanzania Volume Five Edited by Stephen A Lucas kilichotoka mwaka 1975.



Humo ndugu kazi anazungumzia visa vingi baina ya makabila ya Pwani na Wasukuma.

“Wasukuma na Wanyamwezi walifika Pwani kwa sababu ya Biashara ya Utumwa iliyofanywa na Waarabu na wakifanya biashara zingine.”

Katika zoezi hilo wapo waliochukuliwa utumwa wakatokomea utumwani na wapo waliokimbia njiani na kurudi Usukumani, wapo waliokufa njiani na wapo waliobaki maeneo hayo hayo ya Pwani.

“Wasukuma waliweza kwenda sana Pwani na makabila ya Pwani yaliyoweza kufika bara lakini kwa uchache mno, kwa hiyo Wasukuma waliwafahamu mno watu wa Pwani kuliko watu wa Pwani walivyowafahamu Wasukuma na Wanyamwezi, ndiyo maana hadi kesho makabila ya Pwani yanashindwa kuwatafautisha Wasukuma na Wanyawezi.”

Makabila ya Pwani hadi kesho yanaendelea kutowafahamu makabila haya mawili huku nao Wasukuma na Wanyamwezi wanashindwa kwa kiasi kuwatafautisha Waluguru, Wapogoro Wazaramo , Wakwere, Wadoezi na makabila mengine ya Pwani labda wale Wasukuma na Wanyawezi walioishi huku kwa muda mrefu..

Wasukuma waliokwenda Pwani wengine walioa/kuolewa huko na kuzaa na makabila haya huko huko na kufahamu tamaduni nyingi za watu wa Pwani, lakini Watu Wapwani walibaki kuwa maamuma wa Wasukuma na Wanyamwezi waliobaki huku bara.

Ndugu S Kazi  anadai kuwa,

“Watu wa Pwani walipata kazi nyingi baada ya ujenzi wa Reli ya Kati hivyo wengi walipa ajira katika vituo vya Gari Moshi na wengine kuhamia kuhamia moja kwa moja katika maeneo haya ya bara yenye Wasukuma na Wanyamwezi wengi.”

Jambo hilo kidogo lilisaidia sasa Wazaramo , Wakwere na watu wa Pwani kuingia katika kuwafahamu Wanyamwezi na Wasukuma moja kwa moja.



Walipofika Mwanza walikaribishwa majumbani mwa Wasukuma na hapo walikuta wanyama wanaishi pamoja na binadamu , katika makundi makubwa makubwa.

“Nyie jamaa vipi! Mbona mnaishi na Nyati, hawana madhara ? Je hawawezi kuwachoma na pembe zao ?”

Wasukuma hata walipowakaribisha Wazaramo hapa majumbani mwao walikuwa waoga na ng’ombe walipokuwa jirani hapo hapo walikimbilia ndani ya nyumba za Wasukuma na kujificha, huku wakigoma kutoka nje.

S. Kazi anasema,

“Uwoga huo wa Wazaramo kwa mifugo ya bara ulisababisha hata wakati mwingine Gari Moshi liliwapita na kuwaacha na hivyo kugonga Gari Moshi lingine na wakati mwingine walipoteza kazi kisa uwoga wa nyati( ng’ombe)”

Mwanakweu siku ya leo anasema nini?

Ndugu zake Mwanakwetu mara zote wanaogopa nyati anayeishi nyumbani kama anavyosimulia  ndugu S Kazi hivyo ili wawe salama na wasichelewe kupanda Gari Moshi ni lazima wawe na Msukuma kando maana anakulinda na nyati hao, hofu ni zile pembe za nyati hao wanaofugwa majumbani.

Mwanakwetu ndugu zake hawako tayari kupanda Gari Moshi lingine na hawataki kulipa nauli mara mbili, wanataki kuwahi Gari Moshi kwa wakati ule na tiketi ile ile.

Mwanakwetu Upo?

Msukuma Hodari Kukaa na Nyati.

Nakutakia Siku Njema.

makwadeladius@gmail.com

0717649257




 

0/Post a Comment/Comments