Adeladius Makwega-MWANZA
Chuo Kikuu cha Dodoma kinatarajia kufanya mahafali yake ya 14
hivi karibuni, baada ya wanachuo wake kadhaa kufuzu katika kozi mbalimbali za
ngazi kadhaa ikiwamo Shahada, Shahada za Uzamili na Shahada za Uzamivu .
Kulingana na taarifa iliyotolewa kwa umma na chuo hiki inanadi
kuwa,
“Umma wote unajulishwa kuwa majina yafuatayo ya wanachuo wetu
wamefuzu vigezo vyote vya taaluma na watapewa shahada zao katika mahafali hayo ya 14 chuoni hapa.”
Mwanakwetu alipofuatilia orodha hiyo
alibaini kuwa kwa ngazi ya shahada ya uzamivu kulikuwa majina sita,
“Sinyati Ndiango ambaye atatunukiwa Shahada ya Uzamivu ya Falsafa
na wengine watano ambao ni Phesto Namayala, Mwaija Ngenzi, Deodatus Kazawadi,
Thobias Mwesiga na Raymond Mukulasi Chrales.”
Mwanakwetu alipoendelea kusoma orodha
hiyo, namba 51 alikutana jina la mh.Ridhiwani J.Kikwete ambaye hadi sasa ni
Waziri Mdogo wa Tanzania anayehusika na masuala ya utumishi na katika mahafali hayo ya 14 atatunikiwa Shahada ya Uzamili ya
Mahusiano ya Kimataifa.
Mwanakwetu anapongeza wahadhiri wote
waliofanya kazi hiyo kwa haki na bila upendeleo wowote ule, anawaomba waendelee
na moyo huo.
Kwa namna ya pekee Mwanakwetu
anampongeza mhe. Kikwete kwa kufuzu vigezo hivyo vya kuhitimu mafunzo hayo na
anamtakia mahafali mema.
“Elimu hiyo uitumie katika kuwatumikia wananchi wa Tanzania,
katika jukumu ulilo nalo sasa.”
Mwanakwetu anaongeza kuwa mhe.
Kikwete afahamu kuwa siasa ili ziweze kufanyika vizuri mheshimiwa huyu
anatakiwa awe jirani na wananchi wanyonge na wao watambue kuwa yupo nao jirani.
“Wizara yako inashida hasa ya kuweza kupenya katika wizara
zingine za umma kutatua kero za watumsihi wa umma kama vile motisha, uhamisho
na upandaji wa madaraja na mishahara, fanyia kazi hayo.”
Katika orodha hiyo ya
wanaohtimu, mhe. Kikwete afahamu,
“Wapo wahitimu ambao wanajiuliza je
vyeti vyao vitatumika lini? na watapata kazi wapi ? Hata wapo wengine ambao watapewa
vyeti katika mahafali hayo na ni
watumishi wa umma lakini vyeti vyao haviwezi kuwasaidia chochote kutokana
na miongozi iliyopo ambayo inahitaji maboresho madogo.Wapo wengine wanahitimu nawe hata nauli ya bodaboda kufika katika mahafali hayo itakuwa ngumu na wapo wengine wanajua kuwa sasa wanahitimu pesa na bodi ya mikopo hawapati tena je wataishije?.Waziri Mdogo wa Utumishi unatakiwa kuvaa viatu vya hao jamaa wote”
Mwanakwetu anamalizia kwa kusema kuwa,
“Mhe Kikwete umehitimu masuala ya
mahusiano ya kimataifa, fahamu kuwa hakuna mahusiano mazuri ya kimataifa kama mahusiano
ya ndani ni mabovu, lazima kuhimizwa zaidi kujenga mahusiano mazuri ya ndani
ya kidugu zaidi kwa kila mmoja wetu.”
Mahafali mema.
Mwanakwetu Upo?
Hongera Ridhiwani
KIkwete.
Nakutakia Siku Njema.
Makwadeladius @gmail.com
0717649257
Post a Comment