WAZIRI HABARI AWE MSEMAJI SERIKALI

 



Adeladius Makwega-MWANZA

Ijumaa ya Novemba 24,2023 Mwanakwetu alipita katika kundi lenye jina MwAnAKwEtU la mitandao ya kijamii saa 5 na dakika 13 ya usiku aliona nakala ya jarida la Nchi Yetu ambalo linatolewa na Idara ya Habari Maelezo.

Kwa wale ambao ni hawalifahamu jarida hilo ni jarida la serikali la miaka mingi, linatolewa na idara hiyo tangu enzi za SHIHATA na wakati huo likitolewa likiwa na rangi nyeusi na nyeupe tu lakini maendeleo ya tekinolojia sasa linaotolewa likiwa la rangi.

Jarida hilo ni namba 801 ambalo limetolewa huku Idara hii ikiongozwa na ndugu Mobhare Matinyi ambaye sasa ndiye mkurugenzi wa Idara hiyo ya serikali. Jarida hilo lina kurasa 12 zenye maandishi ikiwamo matini kadhaa zenye habari na matangazo.

Mwanakwetu alilitazama jarida hilo na kutamani kuona mchango wa umahiri wa mkurugenzi mpya wa Idara hii, akipitia habari moja baada nyingine na hata uteuzi wa picha katika jarida hilo.


Kwanza aliisoma habari hii Dkt. Biteko Akutana na Balozi wa China Nchini Tanzania. Mwanakwetu alipoisoma habari hyo alijiuliza je kukutana kwa Biteko na Balozi wa China kuna maana gani kwa msomaji wa jarida hilo? Cha maana na kikubwa ni kile walichozungumza.

Ifahamike wazi kuwa jarida hili halitoki kila siku, lilipaswa kuwaachia wengine juu ya huko kukutana yaani vyombo vingine vya habari; kama vile redio, runinga na magazeti ya kila siku. Hivyo Idara ya Habari Maelezo ingejikita katika mazungumzo hayo ya China na Tanzania.

Pia kichwa cha habari kinatakiwa kuwa kifupi , chenye maneno machache na cha kuvutia , mathalani

“China Kuboresha Umeme Tanzania.”

Mobhare Matinyi afahamu kuwa habari ni sayansi ya sanaa na uumbaji wa maneno katika sentensi zenye kuvutia kwa msomaji, msikiliza na hata mtazamaji, hapa hatuandiki kama mtu anaomba kazi. Hapa ni sanaa ya maneno.

Jambo la pili ambalo Mwanakwetu alijiuliza, hivi kulikuwa na haja gani ya jarida hilo kuficha jina la mwandishi wa habari hizo na kuandika MWANDISHI WETU?




Mwanakwetu anasema kuwa yeye anahisi kuwa habari hizo zimeandikwa na Mobhare Matinyi mwenyewe na jina hilo limefichwa makusudi na kwa faida binafsi.Ifahamike wazi kuwa jina la mwandishi mara nying linafichwa katika habari za uchunguzi ili kumlinda na shida yoyote baadaye. Kwa hakika tangu jarida hilo lianze halijawahi kufanya habari za uchunguzi na hata habari zote mbili zilizoandikwa kwa kuficha jina la mwandishi hazina shida yoyote kwa mwandishi na habari , jina lake likifahamika labda woga kukosolewa.

Hata tukihoji ilikuwaje ukaficha jina la mwandishi ,majibu hayapo.

Habari ya ya pili ambaye jina la mwandishi limefichwa ni Dkt. Biteko Akutana na Menejiment ya NMB, ukiisoma habari hiyo ni pongezi tu kwa Naibu Waziri Mkuu, kwa hakika huo mwezi Novemba 2023 pongezi kwa kiongozi huyo hazina maana yoyote kwa msomaji wa jarida la umma ,hapo kama kungekuwa na hoja ya mazungumzo ya maboresho ya NMB, kweli hoja hiyo ingekuwa habari kwa umma wa Watanzania kwa jarida linalotoka kwa muda fulani, kidogo pongezi zilikuwa na tija katika redio, runinga na magazeti yanarusha habari na matangazo  ya kila siku na siyo Nchi Yetu.



Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo atambue kuwa jarida hilo ni la umma na hauwezi kuweka habari mbili za kiongozi mmoja , nchi hii ina viongozi wengi, basi agejitahidi mtu mmoja habari moja na hata habari zenyewe zingekuwa na uzito, huku siku hiyo hiyo na siku zilizotangulia kukiwa na habari tele zenye uzito kutoka taasisi mbalimbali za umma.

Shida nyingine kubwa ipo katika matumizi ya picha, unapoyatazama matumizi ya picha ya jarida hili, Rais hakuwa na habari yoyote zaidi yakutajwa tu katika habari hizo na tena kidogo, kwa hiyo haikupaswa picha yake kutumika kabisa kulitambulisha jarida hilo.

Picha za viongozi zimetumiwa sana, jarida hilo linapaswa kusomwa na wananchi na kila kinachoonekana hapo kijenga dhana ya kueneza mazuri ya serikali . Picha zote 12 ni picha mbili tu zenye nafuu na hata zenyewe hazielezi sana mazuri ya serikali.



Katika matumizi hayo ya picha kunaonekana udhaifu mwingine wa Mkurugenzi wa Idara hii kwa kuingiza picha yake katika jarida hilo.

“Jitahidi kuweka picha za kazi za umma na kupunguza picha za viongozi ili kusaidia serikali iweze kusemewa kwa kina .”

Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo ajitahidi mno kwa kuwekeza nguvu ya umahiri katika kufanya kazi katika idara hiyo. Umahiri huo utasaidia sana kufanya kazi kwa ufanisi ili serikali yetu iweze kusemewa vizuri na kufikia shabaha zake.

Mobhare Matingi atambue.

“Hatuwezi Kulenga Shabaha Namna Hiyo.”

Kinyume chake watu watasema,

“Idara ya habari ya Maelezo ivunjwe, alafu watumishi wa idara hiyo, nusu waende TSN wale wenye ujuzi wa habari za magazeti kidogo na nusu waende TBC wale wenye ujuzi wa utangazaji na ufundi mitambo. Alafu msemaji wa serikali abaki Waziri wa Habari, atafutwe bingwa mmoja awe Waziri wa Habari na Msemaji Mkuu wa Serikali, Hapo Mchezo Kwisha.”

Mwanakwetu anasema,

“Bado anautafuta umahiri wa Mobhare Matinyi katika tasnia hii.”

Mwanakwetu Upo?



Hatuwezi Kulenga Shabaha Namna Hiyo

Waziri Habari Awe Msemaji Serikali

Nakutakia Siku Njema.

makwadeladius@gmail.com

0717649257





0/Post a Comment/Comments