JAMANI HESHIMUNI WAKUBWA NA WADOGO

 



Adeladius Makwega-MWANZA

Mwanzoni mwa mwaka 2023 Kanisa unaloliona hapo juu lilipata mwanakondo (muumini) mgeni, walimkaribisha vizuri na kukaa naye, kanisa hilo ni madhehebu ya Kisabato ambayo huwa wanasali siku ya Jumamosi.

Mwanakondoo huyu alikuwa ni mtumishi wa umma, alipokelewa vizuri na kutambuliswa mbele ya wenzake na maisha ya kituo hicho kipya cha kazi kuanza; kazini, nyumbani na kanisani.

Ndugu huyu alikaa na wenzake vizuri huku akishirki kutoa michango ya imani yake kama miongozo ya dini ilivyo.



Mwanakwetu kwa hakika alivutiwa mno na maisha ya ndugu huyu ya kiroho, akiwa mshika dini wa kweli, katika kufuatilia hilo kama mwanahbari Mwanakwetu alibaini jambo,

“Kuna wakati baadhi ya waamini wenzake walimuomba mchango na yeye kuwapatia mchango huo wa kiroho. Ilikuweza kuupa nguvu mchango huo ndugu huyu aliomba eneo la kilimo kazini kwake na kukubaliwa yeye na watumishi wenzake kadhaa wakapewa eneo kubwa karibu ekari 20 na kulima mazao mbalimbali kama vile mahindi, karanga, maharagwe na choroko. Ndugu huyu aliamua kulima shamba kama ekeri tatu na kupanda mazao kadhaa na akajiuluiza yeye hapo hana familia, mazao hayo hata akivuna yatakuwa mengi , hivyo akaamua shamba hilo baada ya kupanda kuwakabidhi baadhi ya waamini wenzake , wayapalilie vizuri alafu wakivuna wauze na watunishe mapato ya kanisa.”

Mwanakwetu kila alipopita eneo hili alikutana na waamini wengi wakilima kwa umoja kuyapalilia na palizo ya kwanza kwa shirika kila mmoja akiwa na kipande chake, kazi hii ilifanyika vizuri na mahindi hayo kupendeza mno, hadi Mwanakwetu akayaonea gere.


Wakati zoezi la kuyafyeka mahindi likiendelea

Mwanakwetu aliwauliza na majibu yao yalikuwa, yule tunasali naye, mahindi haya tukivuna ni yetu, ametupatia. Mahindi hayo yakawa yanaendelea vizuri .

Kumbuka hili eneo lililolimwa shamba ni eneo la taasisi ya umma, Disemba 24, 2023 limetolewa agizo kuwa kuna kampuni ya Wachina inajenga mradi , hivyo mahindi hayo karibu ekari 20 yakatwe mara moja, ili mradi huo uanze mara moja.

Vijawa wakataji walipewa kazi, wakayafyeka yale mahindi yaliyokuwa katika hatua tatu tofauti; baadhi yalihitaji majuma mawili kukomaa, baadhi yakiwa yatafuta mbelewele na baadhi yakiwa yanahitaji palizi moja tu yatoe mbelewele, hapo bila ya kutaja hali ya choroko, karanga , maharagwe , alizeti na mazao mengine.

Mwanakwetu aliposogea eneo la tukio alikutana na zoezi ufyekaji wa mahindi, hapo alikutana na taswira ya masikitiko makubwa.

“Jamani ulimwengu huu mnayafyeka mahindi ya watu! Mmeshindwa kuzungumza nao?”

Mwanakwetu alijiuliza,

Kando ya eneo hilo palikuwa na kijana wa kiume kijana na mdogo wake eneo lenye  mazo yao lilikuwa ndilo linafyekwa.

“Hawa jamaa wanakata mahindi yetu, mama aliomba ruhusa kulima chuoni, akaruhusiwa , haya mahindi yangekutana na siku 20 yangekomaa lakini wamekata, mama kapigiwa simu anakuja alikuwa gulioni, mimi nimetangulia na mdogo wangu huyu mdogo. Wachina wanasema tukiendelea kukaa hapa watatukamata.”

Hilo ni tukio la kusikitisha sana ambalo Mwanakwetu ameliona kwa macho yake jumapili ya Disemba 24, 2023.


Umefyeka mahindi ya watu alafu unaruhusu trekta la mtu kubeba mahindi yaliyokatwa

Mwanakwetu anashauri yafutayo kwa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,

Mosi, baadhi ya viongozi wamepewa dhamana na Rais Samia Suluhu Hassan lakini dhamana rais inaichezewa shere, mtu makini, muugwana, mstaarabu hawezi kuto ruhusa ya kufyeka mahindi ya watu bila ya kuongea nao kwanza.

Huo mradi unaojengwa siyo mali yako au mali ya familia yako bali ni mali ya hao hao waliopanda mahindi, zungumza nao vizuri , malizana nao alafu endelea na mradi.

Aliyetoa agizo la kuyakata mahindi hayo anaweza kuyapanda mahindi au mazao hayo yakaota ndani ya siku tatu na yakafike hatua yalivyokuwa?

Iwe taasisi ya umma, iwe taasisi binafsi inawajibu kwa kuwaheshimu wananchi na hata wafanyakazi wa ngazi za chini.


Hali ya mahindi kabla ya kufyekwa

Swali ambalo Mwanakwetu anajiuliza yupo kiongozi , awe mkuu wa taasisi, mkuu wa wilaya , katibu mkuu wa wizara yoyote anaweza kuthubuti kuyakata mahindi ya wanakijiji ambapo rais anatoka/ anazaliwa?Yupo kiongozi wa taasisi, wilaya au wizara anaweza kuyakata mahindi ya wazazi wake kijijini bila kuzungumza nao?

“Tuheshimu wakubwa na wadogo.”

Mwanakwetu anashauri suala hilo lichunguzwe mara moja, viongozi waliohusika na tukio hilo wachukuliwe hatua mara moja, kampuni ilivofanya hivyo na hata vijana walifanya uharibifu huo kwa maagizo ya wakubwa wachukuliwe hatua na wakulima hao walipwe fidia ya uharibifu huo ikiwamo waumini wa kanisa la Wasabato hapa Malya.

Mambo ya watu yajadliwe katika vikao pawe na muhtasari mwisho wafikie uamuzi, inawezekana jambo hilo linafanywa makusudi kwa sababu maalumu, lichunguzwe mara moja.Tanzania ni nchi ya watu wa aina zote na hata miradi ni mali ya watu, ukiwa kiongozi wewe ni karani na unafanya kazi hiyo kwa niaba ya watu, ndiyo maana likitokea lolote kwako binafsi kazi inaendelea.

Nakukumbusha kuwaheshimu wakubwa na wadogo.

Nakutakia siku njema.

makwadeladius@gmail.com

0717649257



Shamba wazi baada yamahindi kufyekwa

0/Post a Comment/Comments