Adeladius Makwega-MWANZA
Tangu uteuzi wa Dkt Emmanuel Nchimbi kuwa Katibu Mkuu wa Chama
cha Mapinduzi, Mwanakwetu hakutaka kuandika chochote juu ya kiongozi huyu
mahiri wa Tanzania ambaye amewahi kuwa Waziri katika Wizara kadhaa , Balozi na
hata kuwa Mwenyekiti bora wa Umoja wa Vijana wa CCM Taifa UVCCM.
Lakini asubuhi ya Januari 18, 2024, macho ya Mwanakwetu
yalishuhudia picha moja nzuri ikionesha mabalozi wawili yaani Balozi Hoyce Temu na Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi. Kwa
Mwanakwetu hawa ndugu wote wawili ni viongozi anaowapenda kutoka moyoni, anawakubali
, hivyo aliamua kukuza zaidi picha hiyo na kuwaona vizuri ndugu hao wawili.
Balozi Temu alivalia gauni lenye rangi ya kijivu -nyeusi
likiwa na visanduku na kichwani kwake kavaa kilemba huku akiwa amefumbata mikono
, fumbato hilo la mikono la Balozi Temu lilisindikizwa na tabasamu kubwa.
Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi ambaye sasa Mwanakwetu
anamtambua kuwa ni Katibu Mkuu -Mwenyekiti, hilo jina nitalieleza baadaye,
Katibu Mkuu.... Balozi Dkt Nchimbi amevalia shati jeupe lenye vidoti vidoti
vyeusi na huku akivalia suruali nyeusi.
Alipoikuza zaidi picha hiyo Mwanakwetu aliona kuwa ahaa kumbe
Katibu Mkuu- Mwenyekiti sasa nywele zake zina mvi. Nayo mazingira nyuma ya picha
hiyo yalikuwa mazuri sana na yalipendeza mno machoni paa Mwanakwetu.
Chini ya Picha ukurasa huo wa Instagram wa Balozi Temu alimpongeza Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi
kuteuliwa kuwa katibu Mkuu.
Mwanakwetu alitiririka na maoni katika ukurasa huu na kuna
jamaa mmoja anaitwa Masaweessau yeye
aliibuka akisema sasa chama cha nimoto alafu akaibuka mwingine kutoka huko
alipo ndugu Ussiankhomawa,
“Pongezi nyingi sana
kwa Balozi Dkt. Nchimbi, huu ni moja ya teuzi moto moto moto, Mungu wetu
amsimamie.”
Mwanakwetu alipokuwa akiutazama ukurasa
huu wa instagram wa Balozi Temu akakumbuka baadhi ya maneno ya ya awali ya
Katibu Mkuu-Mwenyekiti Balozi Dkt Emmnauel Nchimbi aliyoyasemba punde alipoteuliwa
tu .
“... Nafasi ya Katibu
Mkuu wa chama chetu, siyo nafasi nyepesi na haina majukumu mepesi maana sisi
ambao tumeanza kuifuatilia tangu inaanzishwa toka mwaka 1982 , tulipoamua
kuachana na Katibu Mtendaji na kuwa Katibu
Mkuu wa Chama, maana awe mtendaji na mwanasiasa tumeipa uzito nafasi hii...
Kuna watu wengine wanasema Nchimbi kuna wakati mwingine ana
misimamo hivi, eee ni kweli kwenye mambo ya msingi mimi nina misimamo na hili
lazima tuelewane na kama mkitaka kunitimua kwa misimamo nitimueni leo ...eee kwenye
mambo ya msingi lazima uwe na msimamo na ndiyo moja ya viapo vya chama chetu, MwanaCCM asiye na msimamo wewe ni ndumila
kuwili, Undumila kuwili siyo sifa ya kuwa mwanaccm.
Nitasimulia hizo habari eee, mwaka 2005 eee.. mzee Mohahamed Gharibi
Bilali alipokuwa anataka kugombea Urais wa Zanzibar, maana wakati ule tulikuwa
na Rais wa Zanzibar Amani Abeid Karume, ameshamaliza temu moja anakwenda temu
ya pili, alikuja kuniona kuniomba nimuunge mkono kugombea , ili yaani Amani Abeid Karume amalize temu
moja aende zake off-course mimi napenda sana watu wenye akili, kwa hiyo
Mohammed Bilali ni moja ya watu ninawaopenda sana , nilipata nafasi ya
kuzungumza naye kwa kituo, wakati huo nilikuwa na miaka 34 nikamwambia mzee...
maana alinieleza anachotaka kuifanyia Zanzibar yaani unasisimka akieleza, nikamwambia
ukweli nimesisimka na maelezo yako lakini siyo utamaduni wetu, ni kweli nimesisimka
lakini siyo utamaduni wetu, tukikupa temu moja tunakuacha unamalizia ya pili kwenye
nafasi ya urais. Sasa nimesema mapema ili tusije tukaelewana vibaya baadaye
eee... CCCM- CCM-CCM-CCM...”
Mwanakwetu yupo katika ukurasa wa
Instagramm wa Balozi Temu na picha yake hiyo juu ilimkumbusha maelezo hayo juu
ya Balozi Dkt Emmanuel Nchimbi Katibu Mkuu mpya wa CCM Taifa.
Mwanakwetu anasema nini siku ya leo?
“Katika hilo la tusije kuelewana vibaya Katibu Mkuu wangu
Balozi Dkt Emmanuel Nchimbi nimekuelewa vizuri na hatutaki kugombana na wewe.”
Mwisho Mwanakwetu anasema kuwa Balozi
Dkt. Emmanuel Nchimbi tunakuita Katibu Mkuu - Mwenyekiti kwa kuwa wewe uliwahi
kuwa mwenyekiti wetu wa UVCCM, kwa hiyo hatuwezi kukupokonya nyota yako ile ya
Uenyekiti wa UVCCM wa wakati ule , japokuwa sasa una mvi , nyota ile itabakia
pale pale ilipo.
Mwanakwetu Upo
Kumbuka tu mwanaccm asiye na msimamo
ni ndumila kuwili
Nakutakia siku Njema.
0717649257
Post a Comment