MWANEGELE 2024 SIYO HATA ISIMANI 2004

 



Adeladius Makwega-MWANZA

Siku ya Januari 26, 2024 ilianza kwa hali ya hewa ya jua, hakukuwa na mawingu, japokuwa mwezi huo ulikuwa msimu wa mvua za masika hapa mkoani Mwanza.

Mwanakwetu alitoka nyumbani kwake, begi lake mgongoni akielekea katika majukumu yake ambayo siku hiyo yalifanyika katika eneo lenye umati mkubwa wa watu.

Mwanakwetu akiuchapa mwendo, akitumia TZ NYAYO, hatua kwa hatua, mara alisikia sauti ikiita.

“Baba, Baba Baba, Mzee Mzee.”

Mwanakwetu alipogeuka tu, alikutana na sura na kijana mmoja, aliyevaa sare za Shule ya Msingi, shati jeupe na kaptura ya rangi ya khaki, chini akiwa amevaa yeboyebo za rangi ya uaridi akiwa amepanda baiskeli.

“Mzee umeangusha kitabu chako, pale juu, twende ukakichukue, mimi nilikuwa naenda shule, nimeona wakati unadondosha .”

Kweli Mwanakwetu alirudi nyuma hadi aliopoingusha kitabu hicho, akiwa na kijana huyu mdogo , kijana akaikota kumbe ni shajara nyeusi na kumpa Mwanakwetu.

“Shajara hiyo ilikuwa ya mwaka 2024, ilichomoka katika begi lake, ambalo hakulifunga zipu yake vizuri, ikiwa ndani yake kuna nyaraka yake muhimu ya thamani.”

Mwanakwetu alimshukuru sana kijana huyu aliyejitambulisha kama RENATUS EMMANUEL mwanafunzi wa SHULE YA MSINGI MWANAGELE, wilayani Maswa, mkoani Simiyu.

Kutokana na kitendo hicho Mwanakwetu alijifunza Jiografia ya Kijiji cha Mwanegele, inaonesha kuwa kijiji hichi kinapakana na Kijiji cha Malya Kilichopo Wilaya ya Kwimba Mkoani Mwanza., ambapo hapo awali MWANEGELE na Malya vyote vilikuwa vijiji vya Wilaya ya Kwimba mkoa wa Mwanza.



Mwanakwetu alibaini kuwa kijiji hiki kina shule za msingi nne na shule za sekondari mbili zinazohudumia wananchi wa Kata ya Nyabubinza, huku watu wa Mwanegele na Malya wakishirikiana vizuri tangu enzi.

“Hapa tuna zahanati yetu nzuri, tunapata huduma vizuri , japokuwa awali wahudumu hawa wa afya walitusumbua lakini sasa hali hiyo imebadilika, tunamshukuru Mungu”

Mwanakwetu alibaini kuwa kijiji hiki tangu enzi ni cha wakulima na wafugaji, awali kulikuwa na wafugaji wengi lakini ugonjwa SOTOKA ulihatarisha mifugo mingi na wafugaji wengi kuondoa katika eneo hilo.

Changamoto cha kijiji hiki anachosoma kijana Renatus Emmanuel ni kutokuwepo kwa maji safi na salama, kijiji hiki kinacho mtandao wa mabomba na chanzo cha maji lakini maji yanatoka mara hache haya wekwi dawa yoyote ile kutoka bwawani yanatoka kama yalivyo.

Mwanakwetu siku ya leo anasema nini?

Kwa hakika kwa umri wa Mwanakwetu amewahi kufanya kazi katika mazingira magumu sana na ya vijijini sana nchini Tanzania kwa vipindi tofauti.

“Mathalani mwaka 2003-2009 aliwahi kuishi Kijiji ch Ujamaa Isimani-Iringa Vijijini Mkoani Iringa, mazingira yake yalikuwa magumu na upatikanaji wa maji ulikuwa kwa wiki maji ya bomba yalitoka mara mbili, lakini kizuri maji hayo ambayo yalikuwa yanatoka mara mbili yalikuwa yanawekwa dawa, haya ni ya mkoani Iringa.

Huu ni mwaka 2024 miaka ishirini baadaye, hali ya maisha ya wanakijiji Cha Mwanegele ni gumu, japokuwa kuna mfumo wa maji lakini maji hayawekwi dawa yoyote ile, hilo ni hatari kubwa kwa afya ya binadamu na uhai wa maisha ya binadamu.

Shida ya Kijiji cha Mwanegele, hiyo hiyo ndiyo shida ya Kijiji Cha Malya ambacho Mwanakwetu anaishi, Mamlaka husika zinatakiwa kujitathimini kwa kuyaangalia maeneo ambayo yana miradi ya maji jamani wekeni dawa.

Hii ni SIMIYU na MWANZA ya 2024 jirani na Ziwa Victoria, Watanzania wanakunywa maji yasiyowekwa dawa? Ambayo hailingani na hata IRINGA ya 2004? Vipi kipindupindu na magonjwa mengine ya tumbo kwa wanavijiji hawa?”

 

Mwanakwetu hamfahamu Mkuu wa Mkoa wa Simiyu angeweza kuwambia neno lakini Mungu Bahati anamfahamu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza ndugu Amos Makalatangu akiwa UVCCM, Waziri Mdogo wa Michezo, wakati Mkuu wa Mkoa enzi ya Rais Magufuli, wakati ukuu wake wa Mkoa unatenguliwa na hata wakati anarudishwa Ukuu wa Mkoa na Rais Samia, namuonba ndugu yetu Amos Makala afuatilie suala la maji katika kijiji cha Malya yatoke kwa wakati na maji hayo yawekwe dawa na viongozi wa SIMIYU walitatue hilo la maji ya Kijiji cha Mwanegele.




Mwanakwetu anaweka chini kalamu yake kwa heshima zote kwa mwanafunzi Renatus Emmanuel wa shule ya Msingi Mwanegele, ambaye wema wake ulimsaidia kumuongoza kufahamu haya ya shida ya maji kwa vijiji hivi vya Tanzania.

Mwanakwetu upo?

Kumbuka MWANEGELE 2024 SIYO ISIMANI 2004

Nakutakia Kwaresma Njema.

makwadeladius@gmail.com

0717649257





0/Post a Comment/Comments