MIMI WEWE WATETEZI MUUNGANO.

 



Adeladius Makwega-MWANZA

“Mwana wa pakaya! Siku inapita, bila ya kuona makala yako ya miaka 60 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar? Mbona nimesona makala kadhaa zenye maudhui mengine?

Mwanakwetu anaulizwa maswali hayo mawili yaliyomo katika jozi moja ya maswali pacha inayohitaji majibu yake.

Mwanakwetu alipokea jozi hiyo ya maswali, kwanza aliyatuliza gambani mithlili Michael Platine, alafu akaja na kicheko. Ndugu huyu muuliza jozi ya maswali alihoji kicheko hicho cha Mwanakwetu.

“Kwani ninasema uwongo? Leo ni Aprili 26, 2024, ukihesabu tangu Aprili 26, 1964 hadi leo ni miaka 60, hayo makumi sita ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Sasa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ina mvi na uwalaza juu yake.”

Mwanakwetu alijibu kwa utani kuwa sasa Jamhuri imevaa wigi. Jamaa akacheka sana.

Mwanakwetu akaongeza maneno haya,

“Natambua hizo kumi sita lakini nilijipa nafasi ya kusoma makala za waandishi wengine, mimi sina la kusema.”

Ndugu huyu akauliza maoni ya Mwanakwetu yakoje kwa miaka hiyo 60 ya taifa lake? Kutokosa la kusema kwa Mwanakwetu ni kukosa uzalendo , Mwanakwetu aliambiwa.

Hapa Mwanakwetu alicheka sana alafu alimsimulia ndugu huyu visa viwili baina ya Watanganyika na Wazanzibari.

“Kuna wakati hawa tunaodai ni Watanzania walikuwa wanafanya kazi nje ya nchi, katika taasisi hiyo waliyokuwa wanahudumu, hawa Wazanzibari walikuwa wengi huku Watanganyika walikuwa wachache, makadili yalikuwa ni 10 kwa 3.

Hawa Wanzanzibari mwenyezi Mungu aliwajalia walikuwa ndiyo washika usukani wa taasisi hii huku wakiunyonga vilivyo nao Watanganyika ndiyo utingo huko huko ughaibuni.Mzungu akawaamini hawa Watanzania kutoka upande wa visiwani wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Katika taasisi hiyo walikuwepo raia kadhaa wa mataifa ya Afrika kama vile Kongo, Kenya, Rwanda, Burundi, Komoro, Madagaska ,Uganda na Somalia Kwa hakika idadi ya Watanzania ilikuwa kubwa watumishi zaidi ya 13 huku haya mataifa ya Afrika yakidonoa nafasi ya mtumishi kati ya 1-3.Huku mataifa mengine yakiambulia sufuri. Hawa Watanzania wakaanza kubaguana huyu anatoka Zanzibar anapewa ajira huyu anayetoka Kilimanjaro anapigwa mkasi. Ikawa heri ajira apate raia kutoka mataifa mengine kuliko Mtanzania mwenzao. Jambo hilo lilikuwa linalalamikiwa kwa siri kwa maneno ya hapa na pale lakini hali ilikuwa hivyo hivyo.Watanzania wanashitakiana ‘Ohh huyu kaukana uraia lakini bado anamiliki nyumba Pemba na Tanga.Waswahili wanasema, ‘Mwana akiwa na Kidonda Mjukuu huwa na kovu.’ Mwisho wa siku nafasi zote juu zikajazwa na raia wa mataifa mengine ya kando ya Tanzania.Hawa raia wa mataifa kando ya Tanzania wanasema waziwazi ‘Watanzania wana mambo yao ya zamani, bado wameyabeba moyoni, nafasi hizi zilikuwa zao ngoja sasa tuwatawale. Wanatumia kibali cha kusafiria kimoja lakini hawaelewani, ngoja wagombani na wakiwa huko chini na waumizane vizuri.’

Hoja siyo tu ya Mtanganyika na Mzanzibari bali hata ya Muunguja na Mpemba .

‘Wanadai kuwa huyu Mpemba anafungua barua zao katika pigion Box zao, wamefikia hadi kiapo kwa kuapa kwa kuipiga chini tasbihi, hawa ni ndugu na tena wa dini moja, Watanzania Pendaneni Jamani.

Mpo Ugenini.’

Jamaa akauliza kwa hiyo mchezo ukaishaje?Mwanakwetu akajibu kuwa ndivyo hivyo Ufalme Umehamia Kwingine. Huyo Mpemba tena alikuwa ameoa mama wa Kindengereko, chuki tele,huku Waafrika wenzao wameshauchukua ufalme, kurudi majaliwa. Jamaa huyu akamuuliza Mwanakwetu sasa hapa shida ipo wapi? Mwanakwetu akajibu kuwa kosa ni la Mwalimu Nyerere,

“Muungano wa Tanganyika na Zanzibar tumeungana, huyo kapoteza vyote huyu kapoteza kidogo, hapo ndipo Nyerere alipobugi(alipotea).Tulitakiwa kama kupoteza tunapoteza wote alafu tunaungana.Kama wewe tunaungana na mimi ukibaki na chee na mimi nabaki na chee.

Mwanakwetu akamuongozea ndugu huyu kisa cha pili;

“Kuna jamaa alikuwa anasafiri kutoka Mwanza kuelekea Tanga, hivyo alipanda basi hadi Arusha Mjini, siku hiyo basi hilo lilikuwa bovu lakini saa tano ya usiku walifika Arusha Mjini. Walipofika Arusha  tu akapanda coaster hadi Moshi usiku huo huo maana alikuwa anawahi shughuli ya Komuniyo ya mtoto wake, hivyo usiku huo saa saba na ushehe alikuwa Stendi Kuu Moshi Mjini, jamaa alikaa saa kadhaa akashauriwa kama anakweda Tanga apande boda boda hadi Njiapanda ya Himo hapo hapo akakata shauri na kupanda bodaboda kwa shilingi 10,000/=akabebwa hadi Njiapanda ya Himo,

kama saa tisa kasoro ya Alfajiri alipofika hapo Njiapanda ya Himo tu akapanda lori ambalo lilikuwa limetoka kushusha saruji na kuomba alipe shilingi 12,000/= hadi Mombo akakubaliwa akaingia mbele ya kichwa cha lori hilo kubwa na kukaa nyuma ya kiti cha dereva huku akiambia vua viatu ili asiachafue kiti hicho maana ni kitanda cha dereva safarini, pale dereva akichoka huwa anapumzika.

Ndani ya lori hilo kubwa la mizigo kulikuwa na watu watano dereva mmoja, utingo mmoja na abiria watatu wanawake wawili na mwanaume mmoja.

Dereva wa Lori hilo ambalo ni mali ya kampuni ya saruji akawa anaongea na utingo wake,

‘Hii Safari tumebahatisha, tunarudi kiwandani, unajua sina hakika kama tutapata tena safari ndefu kama hii ya kuleta saruji huku maana safari zilizopo ni kubeba saruji kutoka kiwandani kwenda bandarini- hizo ni safari fupi, kwa muda mrefu kazi ni hiyo kwani ile saruji inayokwenda Zanzibar, huko wanajenga nini? Saruji ni nyingi wana mradi gani mkubwa?

Safari hizi ndefu ndiyo zina pesa bwana, tuombe Mungu tupate safari ndefu.”

Mjadala ukawa mrefu na safari inaendelea, sasa hawa akina mama, mmoja alishuka kati ya Himo na Mwanga na pili kati ya Same na Makanya–Hedaru. Kumbuka msomaji wangu anayesimulia hilo yeye ni miongoni mwa abiria anayeshuka Mombo. Awali huyu anayesimulia aliwauliza wale waliokuwamo katika lori ni wenyeji wa mikoa gani?

“Dereva alijibu kuwa yeye anatokea Mtwara, Utingo Kilimanjaro hawa akina mama wawili ni wenyeji wa Tanga na huyu abiria mshuka Mombo ni wa Morogoro.”

Wa Mombo alipofika tu alishuka huku hawa jamaa wakaendelea na safari yao na kilichoendelea kwa dereva na utingo wa lori hilo la saruji huko kiwandani kama walipata safari ndefu au waliendelea na safari za Kiwandani Forodhani, huyu aliyesimulia hafahamu hilo bali anakumbuka hiyo ilikuwa mwanzoni mwa Augosti ya 2023.



Mwanakwetu anasema nini siku ya leo?

Hivi, inakuwaje hawa watumishi lori la kiwanda cha saruji wanauliza kunajenga nini huko Zanzibar? Na kwanini hawahoji hii saruji iliyobebwa na wao wenyewe na kuipeleka mkoani Kilimanjaro ambao ni umbali mrefu kutoka kiwanda kikubwa cha saruji? Msomaji wangu majibu yake ni mengi;

“Kwanza wanapenda safari ndefu zinaposho tele na pili kwa sasa mtawala wa hii nchi anatokea Zanzibar (Wanasema huko kunajengwa nini?)

Ndugu hawa bila ya kujua huko Zanzibar pengine hata Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Zanzibar pengine ina miradi yake inayohitaji saruji tele kutoka bara na pengine wananunua huko kiwandani au kuna kampuni ia mrdai mkubwa inaujenga huko Zanzibar.”

Kwa hakika visa vyote viwili vinatoa taswira ya huo muungano wa Tanganyika na Zanzibar ulivyo na jamii haziaminiani.Wananchi kwa wananchi na hata wananchi kwa viongozi. Je nani anapaswa kuutetea muungano huu? Je ni maziara ya Mwalimu Julius  Nyerere na Abeid Amani Karume? Je ni maziara ya wale walioshuhudia muungano huu?Je Viongozi walipo madarakani peke yao?Je ni hiyo katiba na sheria za nchi hii? Je mahakama ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Je ni Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania?  Je ni vyombo vya ulinzi na usalama?



Mwanakwetu mtetezi halisi na wakweli wa muungano huu ni kila Mtanzania ambao ni mimi wewe, kubwa viongozi wetu watoe muelekeo wa kurekebisa makosa ya Julius Nyerere na majibu yake ni Katiba Mpya na maamuzi ni mawili tu kama wakurudishiwa arudishiwe na kama wa kupoteza apoteze .

Mwanakwetu Upo?

Kumbuka tu msomaji wangu,

“Muungano huu ni wa walio hai, hauwezi Kutetewa na waliolala maziarana  Mimi na wewe Watetezi Muungano.”

Nakutakia siku njema.

makwadeladius@gmail.com

0717649257

NB Maana ya neno Ziara ni Kaburi



 





0/Post a Comment/Comments