TUAMINI KATIKA MABADILIKO YA WENZETU-PADRI MASANJA

 



Adeladius Makwega-MWANZA

“Mimi ni mzabibu- nyinyi ni matawi yangu, akaaye ndani yangu -nami ndani yake, huyo huzaa sana. Ndugu zangu wapendwa tunaadhimisha jumapili ya Tano ya Pasaka tunaalikwa kukutana na Kristo, tunaalikwa kuonana na Kristo, maana Pasipo yeye sisi hatuwezi kufanya lolote pasipo yeye sisi hatuwezi kuzaa matunda bora, pasipo yeye hatuwezi kuwa na faida kwetu wenyewe na hata kwa watu wengine.”

Hayo ni maneno ya utangulizi ya mahubiri ya Padri Samson Masanja mara baada ya kuisoma injili ya Dominika yaTano ya Pasaka, katika Kanisa la Bikira Maria-Malkia wa Wamisionari-Parokia ya Malya -Jimbo Kuu Katoliki la Mwanza Aprili 28, 2024 .

Padri Masanja alisema kuwa Kristo ambaye ni Mzabibu wa Kweli wakati sisi ni matawi yake na kila Mkristo anatakiwa kuishi katika muunganiko huo., alisisitiza kuwa kama sisi ambao ni matawi yake kama tutaruhusu muungano huo kuvunjwa basi tutatupwa motoni, alirejea maisha ya Sauli mara baada ya kumpokea Kristo alifanya kazi yake vizuri huku akiwa tayari kwa mapambano kwa ajili ya Kiristo ambapo awali Sauli huyo huyo alilihangaisha Kanisa la Kwanza,

“Paulo anabadilika kabisa nakuwa kiumbe kipya na kufanya kazi ya Kristo na hata mitume wanapomuona wanamtilia shaka maana wanazijua kazi zake zote alizozifaya.Upya wa Saulo unakuja baada kuunganika na Kristo.”

Hapa mitume bado wanamashaka hadi Barnaba anaingilia kati kwa kuwaambia mitume mpokeeni.Hata katika maisha yetu tunafundishwa kuamini katika mabadiliko ya wenzetu.



Barnaba anasisitiza,

“Huyu siye Sauli aliyewauwa Wakristo bali huyu ndiye Sauli anayemtangaza Kristo.”

Tukubali mabadilko katika maisha ya wenzetu na uwezekano wa kubadilika ni wa Bwana.Padri Masanja aliongeza kuwa ni jambo gumu kuamini katika mabadiliko ya wenzetu kama ilivyokuwa kwa mitume,

“Unaishi na mtu mwongo kwa miaka kadhaa, unaishi na mtu mwizi kwa miaka kadhaa alafu unamuona amebadilika, hilo linakuwa gumu, nawaomba tuamini katika mabadiliko hayo ya wenzetu.”

Padri Masanja aliufunga ukurasa wa mahubiri yake kwa kusema kuwa hivyo ndivyo Kristo anavyotufundisha kuzifanya kazi zake ambapo anatutaka sisi kuzaa matunda mema,

“Matendo mema yanatokana na imani yetu iliyo thabiti, imani yetu iliyo imara kwa hiyo tutazaa matunda bora”

Misa hiyo pia iliambatana na nia na maombi kadhaa,

 

“Ulisema kwamba yule asiye kaa ndani yako, huyo atatupwa nje na kunyauka, utuimarishwe tusinaswe na kishawishi cha kujitenga nawe –Eee Bwana Twakuomba Utusikie.”

Kwa hakika hadi misa hiyo ya kwanza iliyoanza saa kumi na mbili inakamilika saa moja ya unusu ya asubuhi, hali ya hewa ya Malya Wilaya Kwimba umbali wa karibu KM 120 kutoka lilipo Jiji la Mwanza ni jua la kadili, mandhari ya chanikiwiti kila kona nako huko mabaweni(mabondeni) wakulima wakivuna mipunga yao.



0/Post a Comment/Comments