MWENYE NJAA NA KIU ANAWEZA KUHAMISHA UFALME

 



Adeladius Makwega -MWANZA

Novemba 8, 2021 Mwanakwetu alikuwepo katika Kijiji cha Ujamaa Ikangao Ulanga Mkoani Morogoro kushiriki maziko ya babu yake mdogo aliyefahamika kama Otimali Makwega Kazimbaya, Kijiji cha Ikangao kilikuwa hakina umeme hivyo alitoka zake hapo hadi Tarafani Mwaya ili aweze kufanya kazi zake kadhaa katika mitandao pesa na simu.

Maana Kitogoji cha Mrundu na eneo lote la Ikangao hata mtandao wa simu kupatikana ilikuwa tabu.

Akiwa hapo Mwaya , Mwanakwetu aliyaandika makala haya,

Wilaya ya Lushoto wakati huo ilikuwa ikiundwa na Halmashauri mbili nazo ni Lushoto na Bumbuli, huku Lushoto ikiwa ndiyo wilaya katika mwamvuli wa Halmashauri mbili ndugu , Halmashauri ya Lushoto ikiwa na majimbo mawili Lushoto na Mlalo.Nalo jimbo la Bumbuli likiwa na Halmashauri hiyo hiyo ya Bumbuli.

Kwa kukadilia Halmashauri ya Lushoto ilikuwa na watumishi wa umma wenye ajira za kudumu zaidi ya 3500 kutoka idara zote.Katika makala hayo Mwanakwetu aliyanukuu maneno haya kutoka kwake Binafsi,

 

“Nikiwa na athari ya Uongozi wa Vyama vya Wafanyakazi kutoka Shirika la Utangazaji la Tanzania maana hapo nilipokuwa Mwenyekiti wa Wafanyakazi. Unapokuwa mwenyekiti wa wafanyakazi kubwa lilikuwa nikupigia kelele maslahi na posho za watumishi kila mfanyakazi apate kwa usawa. Kila safari iliyokuwa hapa TBC wakati huo zilikuwa ni kwenda Bungeni Dodoma kutayarisha Vipindi vya Leo Katika Bunge, Maswali a Majibu Bungeni, Mijadala Bungeni na Matangazo ya Moja kwa Moja ya Bunge kabla ya huyu huyu Nape Nnauye(Waziri) kusitisha matangazo ya Bunge Live kwa madai kuwa yalikuwa ya gharama kubwa kwa TBC kuyarusha moja kwa moja.

Kwa hiiyo nilipofika Halmashuari ya Lushoto nikiwa bado nina mawazo ya kuhakikisha posho zinatolewa kwa uwiano wa wote na kwa usawa angalau kuonesha kuwa kilichopo kinatolewa kwa wote.”

Mwanakwetu yu Mwaya Ulanga mkoani Morogoro hiyo ni Novemba 2021 kama nilivyokujulisha, aliendelea kusimulia matukio  yq kweli kati ya 2016-2019 LUSHOTO-TANGA na MBOZI-SO.NGWE

“Kuna kijana mmoja ambaye ninamkumbuka kwa jina moja la Japhert, akiwa ni Afisa Utumishi na Rasilimalia Watu wa Halmashauri hii ya Lushoto akiwa na cheo kidogo sana niliongea naye juu ya namna ya kutoa angalau bakishishi/posho kwa watumishi kila wakati wa sikukuu.

Jambo hlo aliniambia kuwa ni gumu sana lakini nilijaribu kushauriana naye tukiwa wawili juu ya namna ya kuweza kutoa bakishishi hiyo ambayo ingekuwa kama motisha kwa watumishi. Nilizungumza naye mengi nikimwambia kuwa ‘Haya mapato tunayosema tumekusanya kumbuka wanaofanya kazi hiyo ni watumishi wa ngazi ya chini kabisa, kuna wajibu wakuhakikisha angalau hata kila sikukuu wao watumishi wa ngazi ya chini kuweza kupata chochote kile.

Kwa utaratibu wa utumishi wa umma namna ulivyo, mkubwa hata kama atalipwa kiasi gani lazima mtumishi wa ngazi ya chini atashiriki iwe kuweka saini, kulibeba faili, kuchapa barua, kufanya uhakiki wa malipo hayo, kuhifadhi hiyo nyaraka au kutuma hizo fedha za kwenye mfumo wa malipo . Kwa hiyo kutoshirikisha watumishi wa ngazi ya chini kupata posho/ bakishishi na stahiki zote za kisheria kunaleta malalamiko mengi na huko si kutenda haki na mtake mistake nyaraka za serikali zitakuwa mitaani.’

Mwisho wa siku tulikubaliana kuwa zoezi hilo linaweza kufanyika kwa kutoa angalau posho/bakishishi kwa kila mtumishi lakini si kwa kutoa pesa bali kwa kutoa kitoweo wakati wa sikukuu za kidini. Jambo hili lilipokamilika nilimuagiza Mkuu wa Idara ya Mifugo wakati huo ambaye alikuwa akifahamika kama Eliezeer Moses ndugu huyu alisema kuwa suala hilo linawezekana kwa kuwa wilaya hiyo ilikuwa na wafugaji wengi basi wangeweza kuwasiliana na kupata wanyama hao ili wachinjwe kwenye machinjio ya Halmashauri.

Kweli tulipozungumza na Bwana Fedha wa Halmashauri zoezi hilo lilikamilika na fedha kutolewa kwa kila sikukuu za dini huku tukishirikiana na wale wanaofanya biashara ya kuchinja mjini hapo na zoezi lilikuwa jepesi ”

Kumbuka msomaji wangu Mwanakwetu yu Mwaya Ulanga Morogoro na hiyo ni Novemba 2021.Mwanakwetu aliendela kuyatayarisha makala yake,

“Kwa hiyo ikiwa kama motisha ya watumishi wote kwa kila Pasaka, Maulidi, Noeli, Idd al Haji na Idd el Fitri. Kila kulipokuwa na sherehe hizo ikawa kama destruri ya kununuliwa ng’ombe kadhaa wakichinjwa na kugawiwa watumishi wa halmashauri hii huku nilibainia kuwa nyama hiyo ilipotolewa watumishi wote wa wilaya hii kutoka taasisi zingine za umma walikuwa wakipewa bila ubaguzi ambalo kwa hakikia lilikuwa jambo zuri na la kujenga umoja na udugu.

 

Nilibainia kuwa hata watumishi waliokuwa na kipato kikubwa waliweza kuchukua kilo mbili hizo za nyama kila sikukuu kwani ilikuwa ni haki yao. ‘Ngoja tukachukue nyama tuliyopewa na mwajiri wetu’.Hayo yalikuwa maneno ya kawaida wakiwalingishia wale ambao siyo watumishi wa umma.Kwa hilo lliwavutia baadhi ya wasio watumishi wa umma kuwa watumishi wa umma.

Kwa hakika Lushoto zoezi hili lilifanyika vizuri na halikuwa na mashaka yoyote huku sikukuu ikifika hata kama mkubwa amesafiri bali alikumbushwa juu ya hilo.

Nyuma ya pazia katika kutoa kitoweo cha kilo mbili za nyama ilikuwa ni kitu muhimu sana kuna wakati wa sikukuu inafika mtumishi hata kama sikukuu si ya dini yake anawajibu wa kupika chakula kizuri ili familia yake iweze kuwa na amani. Kwani nyumba ya jirani pana nukia pilau watoto wa mtumishi wa umma kweli wanakosa chochote?

Wapo wengine ambapo siku za sikukuu uenda kula sikukuu miji mingine makubaliano na vyama vya wafanyakazi yalikuwa wale wasiokuwepo wasichukuliane kwa hoja moja kuwa wao sikukuu hawapo “

Mwanakwetu aliendelea kuyaandika makala yake siku hiyo hapo Mwaya Tarafani.

“Haiwezekani wewe ni kiongozi wa taasi una furaha kubwa wenzako unaowangoza wana shida, dhiki na tabu. Kwa hiyo kila mmoja alipata kitoweo chake, yeye alikuwa na jukumu la kutafuta mchele tu na bei ya mchele ilikuwa kati 1200-2000/= Nyama ilikuwa 6000-7000/- ”

Msomaji wangu tambua hili;

“Katika Bibilia kuna simulizi tele za umuhimu wa chakula mathalani, kumbuka Yesu katika Karamu ya Mwisho aliketi na kula na wanafunzi wake, kumbuka nadhani mtoto wa kwanza Yakobo kupoteza Ufalme hoja ilikuwa ni chakula,kumbuka kisa cha Malkia Sheba na Chakula katika Ufalme wa Wayahudi.

Kuna umuhimu mkubwa katika maisha ya mwanadamu pawepo na upatikanaji wa chakula. Unaweza Kusema Kazi Iendelee/ Hapa Kazi Tu.Je hawa watu wanachakula je wanakula wanashiba?

Watu Wenye Njaa na KiuuWanahamisha Ufalme

Kumbuka msomaji wangu Mwanakwetu yu Mwaya akiandka makala haya.Baadaye ya miaka mitatu Mwanakwetu alihamishiwa Halmashauri ya Mbozi , alifika hapo Agosti 15, 2018.



Anakumbuka alipofika tu baada ya juma moja kulikuwa na sherehe ya Maulidi ya kuzaliwa Mtume Mohammed S.A.W. Kumbuka zile habari za Lushoto uzoefu wake wa kutoa posho hapa alitoa agizo hilo la kununuliwa ng’ombe na kuchinjwa na kugawawiwa kwa watumishi zaidi ya 4000.

Mbozi walienda mbali zaidi kwani angalau kila mtumishi walishauri apatiwe na kilo 2 za mchele na kilo mbili za nyama, hapa posho ilikuwa kubwa.

Msomaji wangu kilo mbili za nyama na kilo mbili za mchele ni karibu shiling 20,000/= hiyo siyo kitu kwa mtu mwenye ukwasi na ni kama upuuzi tu LAKINI KWA AMBAYE FUKARA/MASIKINI / HOEHAE/ PANGU PAKAVU TIA MCHUZI / AKINA YAKHE ambaye fedha hana na tena siku ya sikukuu, hata kama ana mshahara, pengine kaukopea, au anawalipia karo za shule watoto wake kadhaa, Posho ya Nyama na Mchele ni mkombozi wa familia.

Nyuma ya pazia yakizungumzwa haya maneno,

“Duu jamaa kwanini ametoa nyama na mchele kwa watumishi ? Huyu atakuwa anafanya kafara za kwao.

Huyu jamaa ametoa nyama katika sherehe ya dini yake, yeye ni Muislamu ndiyo maana amefanya hivyo kwa Waisilamu wenzake. Hawa waswahili wana shida sana!”

Haya yalisemwa bila hata ya kutambua dini ya wanayemlalamikia. Posho ya nyama na mchele iliendelea kutolewa kila sikukuu za dini na hilo liliongeza motisha kwa watumishi japokuwa ilikuwa vigumu kuweza kuwagusa watumishi wote haswa wale wa vijiji vya mbali na wilaya ya Mbozi lakini ilibainika kuwa wengine walikuwa wakifunga safari kuchukua posho yao Mjini wale wa maeneo yaliyokuwa yakifikika na hapo wilayani.



Hapa ni watumishi ambao walikuwa kata ambazo gharama za kufika Vwawa zilikuwa kwenda na kurudi haifiki 2000-3000/= walikwenda  kwa wingi maana kigezo kilikuwa ni kitambulisho cha kuwa mtumishi wa Halmashauri ya Mbozi tu.

Ikaja noeli tukatoa vizuri posho hiyo na hakukuwa na hoja yoyote, kukawa kimya huku sasa wakibaini kuwa huyu jamaa huwa anatoa posho hiyo posho kila sikukuu na kigezo cha dini kilipotea na wengine walifahamu kuwa huyu ni Mkristo.

Kumbuka unapoona kuwa kimya tambua kuna jambo linaendelea, usindanganyike jambo limekwisha, ilipofika Pasaka ya 2019 maandalizi ya kuwanunulia watumishi ng’ombe na mchele yalifanyika vizuri huku watumishi wakiekezwa pahala pa kuchukua nyama na mchele hapo hapo Halmshauri VWAWA.

Mwanakwetu alikuwa yupo nyumbani kwake huku na yeye akiletewa kiasi ya nyama na mchele na watumishi wa Idara ya Mifugo waliyokuwa wanasimamia zoezi.

Ilipofika saa 12,30 ya asubuhi huku nyama hiyo ikikaribia kugawiwa alijulishwa kuwa kuna sehemu ya nyama ambayo ipo katika machinjo hayo ilikuwa imechinjwa na watu ambao siyo wahusika wa kuchinja. Jambo hilo lilileta taharuki kubwa huku Mwanakwetu akiwasiliana na Shekhe wa Kata ya Vwawa na Shekhe Mkuu wa Wilaya hiyo aliyekuwa akifahamika kama Shekhe Mbwana.

“Nilijulishwa kuwa vijana watatu waliingia katika machinjio hayo na kuanza kuwachinja ng’ombe wa watumishi lakini kwa bahati nzuri Shekhe wa Kata ya Vwawa aliwabaini baadaye suala hilo lilijulishwa kwa viongozi  na nyama hiyo kutengwa na baadaye kugawiwa wahitaji wengine ambao wao wenyewe walihitaji.

Swali lilikuwa nani aliwaruhusu vijana hao kufanya tukio hilo? Waliingiaje katika machinjio hayo wakati kuna walinzi?Nani aliwaagiza kufanya hivyo? Walifanya hivyo kwa manufaa ya nani? ”

Mara baada ya kufanya uchunguzi huo ilikuwa ni kweli kuna vijana waliweza kuingia pahala pa kuchinjia nyama.Walihojiwa na kuchukuliwa hatua kali huku Shekhe Mbwana-Shekh Mkuu wa Wilaya ya Mbozi wakati huo akisisitiza wale wanaosimamia uchinjanji wa nyama kwa mujibu wa taratibu za BAKWATA kuwa makini kuwahi pahala pa kuchinjia na kutimiza wajibu wao ipasavyo na asiyehusika asisogelee eneo la machinjio hayo kabla ya wakati.



Kwa upande wa Halmashauri hii walinzi, Bwana Afya wa Kata na wasimamizi wote wa zoezi hilo walitakiwa kuwa makini maana suala hilo linaweza kuharibu amani na nia njema ya kutoa posho /bakishishi hiyo kwa watumishi.

Mwanakwetu kumbuka alikuwa Mwaya alipomaliza kuyandka makala haya aliyatuma katika vyombo vya habari na kuchapishwa siku zilizofuata.

Mwanakwetu anasema nini siku ya leo?

Mwanakwetu anakumbuka kuwa Mei Mosi ya Kila Mwaka ni siku ya Wafanyakazi Duniani swali ni je kila mwajiri anatimiza wajib wake kuwapa motisha wafanyakazi wake? Shabaha ya makala haya ni kumkumusha kila mwajiri kutoa motisha kwa wafanyakazi wake hasa watumishi wa ngazi ya chini, Waajiri wasijitazame wao wenyewe tu, hilo ni kosa na udhaifu mkubwa.

Mwajiri yoyote anapaswa atambue kuwa  katika kujali maslahi ya wengi kuna vikwazo vingi, maana watu ni wabinafsi,ukiwa mkubwa upe kisogo ubinafsi.

Katika jamii zetu walio wengi wanateseka sana na wanalalamikia mioyoni mwao.

Katika kuwasaidia watu kuna changamoto moja kubwa anaye fanya hivyo anaweza hata kupoteza  hata nafasi yake kwa visa vingi.Mwanakwetu anakwambia usirudi nyuma wewe leo ni mkubwa kesho siyo wewe na siy mwanao, ni mtu mwingine kabisa.

Kumbuka kama hawa waliotuwa kuingia zizini na kuwachinja ng’ombe huku wao wakiwa siyo wahusika na siyo Waisilamu, hiyo yote ni kumrudisha nyuma mtu mwenye nia njema .

Katika tukio hilo waliofanya hivyo hawakutambua mambo mengi ;



mahusiano ya Mwanakwetu na Ustadh Mbwana na pia  hawakutambua kuwa Ustadh Mbwana -Shekhe Mkuu wa Wilaya ya Mbozi alikuwa anafahamiana na Mwanakwetu kabla ya kufika hapo, hawakutabua Ustadhi Mbwana alikuwa anazo taarifa za Mwanakwetu za utoaji wa ruzuku nyakati za sikukuu tangu Lushoto.

Kwa kukuongezea msomaji wangu wakati Mwanakwetu anatoka Lushoto aliwaaga Viongozi wa BAKWATA Wilaya ya Lushoto , akiwamo Katibu wao maana mwenyekiti alikuwa amefariki hawa Viongozi wa BAKWATA walituma ujumbe kwa BAKWATA–MBOZI.

“Huyo jamaa anakuja , ametoka hapa Lushoto, ni mtu mwema , ni Mkristo nawaombeni mkae nae vizuri.”

Mwisho kabisa huyu Ustadh Mbwana Mwenyekiti BAKWATA Mbozi alikuwa alikua mzaliwa wa Korogwe Milimani- Kwa Profesa Maji Marefu, Tanga

Katika jambo hilo msomaji wangu tambua kuwa viongozi wa dini wanayafahamu mengi kikubwa kwa viongozi serikali na waamini waheshimuni sana sana bila kujali wa dini yako au dini ya mwingine, hawa wana taarifa nyingi za maeneo walipo a hata taarifa za viongozi .

Mwisho kabisa Mwanakwetu anasema haya ,

“Anawaomba viongozi wa CCM wa Mkoa wa Songwe shirikianeni na huyu Mkuu wa Mkoa wa sasa ndugu Daniel Chongolo, kwa maana spidi ya maendeleo ya mkoa wa Songwe Mwanakwetu anatilia shaka, shida ni wanasiasa wa kutoka CCM lakini wananchi wa Songwe ni wanapenda maendeleo sana.

Mfano Mdogo Hamashauri ya Mbozi hadi leo hii bado ni Halmashauri ya Wilaya, ipo mkoani! Je walipo sasa wanakusanya mapato vizuri? Mbozi ikiwa Manispaa Mlowo inakuwa Halmashuri ya Wilaya -bajeti ya miradi ya serikali inaongezeka idadi ya watu mnayo, mapato yapo kama yanasimamiwa  vizuri 

 Msaidieni Daniel Chongolo, mjisaidie wenyewe, angalieni maendeleo ya upande wa mpaka kule Zambia oneni gere, lazima Mbozi iwe manispaa ili Mbozi ikutane na Mbalizi.na ikutane na Tunduma.

Viongozi wakifika hapo wanaondoka vibaya kwanini? Kila Mkuu wa Mkoa mbaya? Chiku Galawa alikuwa mkuu wa mkoa Mzuri  ameondolewa W.ananchi wa Songwe wanataka / wanayapenda maendeleo.

Namuomba Dkt Emmanuel Nchimbi itazameni CCM ya huu mkoa na wale waliyopigiwa kura iwekeni vizuri. ”

Kumbuka tu hii,

“Wenye Njaa na Kiu Wanahamisha Ufalme”

Nakutakia Siku Njema.

makwadeladius@gmail.com

0717649257





0/Post a Comment/Comments